18 Na faida yake na malipo+ yake lazima viwe kitu kitakatifu kwa Yehova. Havitawekwa akiba, wala kurundikwa, kwa sababu malipo yake yatakuja kuwa ya wale wanaokaa mbele za Yehova,+ kwa ajili ya kula na kushiba na kwa ajili ya mavazi yenye fahari.+
5 Wakati huo utaona na hakika ung’ae,+ na moyo wako kwa kweli utatetemeka na kupanuka, kwa sababu mali za bahari zitajielekeza kwako; mali za mataifa zitakuja kwako.+
7 Makundi yote ya Kedari+—yatakusanywa pamoja kwako. Kondoo-dume wa Nebayothi+—watakuhudumia.+ Wakiwa na kibali watakuja juu ya madhabahu yangu,+ nami nitairembesha nyumba yangu ya urembo.+