Amosi
9 Nilimwona Yehova akiwa juu ya madhabahu,+ naye akasema: “Kipige kichwa cha nguzo, ili vizingiti vitikisike. Na uvikate vyote kichwani.+ Na sehemu yao ya mwisho nitaua kwa upanga. Hakuna yeyote kati yao anayekimbia atakayefanikiwa kukimbia, na hakuna yeyote kati yao anayeponyoka ambaye atafanikiwa kutoroka.+ 2 Wakichimba chini kuingia katika Kaburi,* toka humo mkono wangu mwenyewe utawachukua;+ nao wakienda juu mbinguni, toka huko nitawashusha chini.+ 3 Nao wakijificha katika kilele cha Karmeli, nitawatafuta kwa uangalifu na kuwachukua kutoka huko.+ Na wakijificha kwenye sakafu ya bahari kutoka mbele za macho yangu,+ huko chini nitamwamuru nyoka, naye atawauma. 4 Nao wakienda utekwani mbele ya adui zao, kutoka huko nitaamuru upanga, nao utawaua;+ nami nitaweka macho yangu juu yao kwa mabaya, wala si kwa mema.+ 5 Naye Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova wa majeshi, Yeye ndiye anayeigusa nchi, ikayeyuka;+ na wakaaji wote ndani yake wataomboleza.+ Nayo yote itainuka kama Nile, na kuzama kama mto Nile wa Misri.+
6 “ ‘Yeye anayejenga ngazi zake huko mbinguni,+ na jengo lake juu ya dunia ambayo ameiwekea msingi;+ yeye anayeyaita maji ya bahari,+ ili ayamwage juu ya uso wa dunia+—Yehova ndilo jina lake.’+
7 “ ‘Je, ninyi si kama wana wa Wakushi kwangu, enyi wana wa Israeli?’ asema Yehova. ‘Je, sikuleta Israeli kutoka nchi ya Misri,+ na Wafilisti+ kutoka Krete, na Siria kutoka Kiri?’+
8 “ ‘Tazama! Macho ya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova yako juu ya ufalme wenye dhambi,+ naye atauangamiza kutoka juu ya uso wa nchi.+ Hata hivyo, sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,’+ asema Yehova. 9 ‘Kwa maana, tazama! Ninaamuru, nami nitaipepeta nyumba ya Israeli katika mataifa yote,+ kama vile mtu anavyopepeta kichujio, lisianguke chini jiwe la mviringo hata moja. 10 Kwa upanga watakufa—watenda-dhambi wote katika watu wangu,+ wale wanaosema: “Taabu hiyo haitakuja karibu wala kutufikia sisi.” ’+
11 “ ‘Katika siku hiyo nitakisimamisha+ kibanda+ cha Daudi ambacho kimeanguka,+ nami nitayarekebisha matundu yao. Na mabomoko yake nitayasimamisha, nami nitakijenga kama katika siku za kale,+ 12 ili kwamba wamiliki mabaki ya Edomu,+ na mataifa yote ambayo juu yao jina langu limeitwa,’+ asema Yehova, anayefanya hayo.
13 “ ‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova, ‘na anayelima atampita anayevuna,+ na anayekanyaga zabibu atampita anayechukua mbegu;+ na milima itatiririka divai tamu,+ na vilima vyote vitayeyuka.+ 14 Nami nitakusanya na kurudisha mateka wa watu wangu Israeli,+ nao watajenga majiji yaliyofanywa ukiwa na kukaa ndani yake,+ watapanda mashamba ya mizabibu na kunywa divai yake, watafanyiza bustani na kula matunda yake.’+
15 “ ‘Nami nitawapanda juu ya nchi yao, wala hawatang’olewa tena kutoka katika nchi yao ambayo nimewapa,’+ Yehova Mungu wako amesema.”