Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 9:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Kwa maana kuna mtoto ambaye amezaliwa kwetu,+ kuna mwana ambaye tumepewa;+ na utawala wa ukuu utakuwa juu ya bega lake.+ Naye ataitwa jina Mshauri wa Ajabu,+ Mungu Mwenye Nguvu,+ Baba wa Milele,+ Mkuu wa Amani.+

  • Isaya 11:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na tawi+ litatoka katika kisiki cha Yese;+ na kutoka katika mizizi yake chipukizi+ litazaa.+

  • Yeremia 23:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 “Tazama! Siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitamsimamishia Daudi chipukizi adilifu.+ Na hakika mfalme atatawala+ na kutenda kwa busara na kutenda haki na uadilifu katika nchi.+

  • Ezekieli 17:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Na miti yote ya shambani italazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova,+ nimeushusha ule mti mrefu,+ nimeuweka juu ule mti mfupi,+ nimeukausha ule mti ambao ungali mbichi+ na kuufanya mti uliokauka uchipuke. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema nami nimefanya+ hilo.” ’ ”

  • Ezekieli 37:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “ ‘ “Na mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme juu yao,+ nao wote watakuwa na mchungaji mmoja;+ nao watatembea katika maamuzi yangu ya hukumu,+ na sheria zangu watazishika,+ nao hakika watazifanya.+

  • Zekaria 12:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Katika siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuzunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ na yeye anayejikwaa kati yao atakuwa katika siku hiyo kama Daudi,+ na nyumba ya Daudi kama Mungu,+ kama malaika wa Yehova mbele yao.+

  • Luka 1:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 na, tazama! utachukua mimba katika tumbo lako la uzazi na kuzaa mwana,+ nawe utamwita jina lake Yesu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki