Zekaria
12 Tangazo:
“Neno la Yehova kuhusu Israeli,” asema Yehova, Yeye anayetandaza mbingu+ na kuweka msingi wa dunia+ na kufanyiza roho+ ya mwanadamu ndani yake. 2 “Tazama, mimi ninafanya Yerusalemu+ kuwa bakuli linalosababisha kuyumba-yumba kwa vikundi vyote vya watu kuzunguka pande zote;+ na pia atakuja kuzingira Yuda, naam, Yerusalemu.+ 3 Na itatukia katika siku hiyo+ kwamba nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe+ lenye kulemea vikundi vyote vya watu. Wale wote wanaoliinua bila shaka watajitia mikwaruzo mikali; na mataifa yote ya dunia hakika yatakusanyika+ kupigana naye. 4 Katika siku hiyo,”+ asema Yehova, “nitamtia mshangao kila farasi+ na kumtia wazimu+ mpandaji wake; nami nitafungua macho+ yangu juu ya nyumba ya Yuda, nami nitampofusha kila farasi wa vikundi vya watu. 5 Na mashehe+ wa Yuda watasema moyoni mwao, ‘Wakaaji wa Yerusalemu ni nguvu kwangu katika Yehova wa majeshi Mungu wao.’+ 6 Katika siku hiyo nitawafanya mashehe wa Yuda kama chombo cha moto kati ya miti+ na kama mwenge wenye moto katika fungu la nafaka iliyokatwa hivi karibuni,+ nao watateketeza vikundi vyote vya watu kuzunguka pande zote upande wa mkono wa kuume na wa kushoto;+ na Yerusalemu litakaliwa tena na watu mahali pake mwenyewe, katika Yerusalemu.+
7 “Naye Yehova hakika ataokoa mahema ya Yuda kwanza, kusudi uzuri wa nyumba ya Daudi na uzuri wa wakaaji wa Yerusalemu usiwe mkuu mno kuliko Yuda. 8 Katika siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuzunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ na yeye anayejikwaa kati yao atakuwa katika siku hiyo kama Daudi,+ na nyumba ya Daudi kama Mungu,+ kama malaika wa Yehova mbele yao.+ 9 Na itatukia katika siku hiyo kwamba nitatafuta kuyaangamiza mataifa yote yanayokuja kupigana na Yerusalemu.+
10 “Nami nitamimina juu ya nyumba ya Daudi na juu ya wakaaji wa Yerusalemu roho ya kibali+ na maombi,+ nao watamtazama Yule waliyemchoma,+ nao wataomboleza juu Yake kama kuombolezea mwana wa pekee; na kutakuwa na maombolezo machungu juu yake kama vile kunapokuwa na maombolezo juu ya mwana mzaliwa wa kwanza.+ 11 Katika siku hiyo maombolezo katika Yerusalemu yatakuwa makubwa, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika nchi tambarare ya bonde la Megido.+ 12 Na nchi hakika itaomboleza,+ kila familia peke yake; familia ya nyumba ya Daudi peke yake, na wanawake wao peke yao;+ familia ya nyumba ya Nathani+ peke yake, na wanawake wao peke yao; 13 familia ya nyumba ya Lawi+ peke yake, na wanawake wao peke yao; familia ya Washimei+ peke yake, na wanawake wao peke yao; 14 familia zote zitakazobaki, kila familia peke yake, na wanawake wao peke yao.+