42 Nami nitalikumbuka agano langu pamoja na Yakobo;+ na hata agano langu pamoja na Isaka+ na hata agano langu pamoja na Abrahamu+ nitalikumbuka, nayo nchi nitaikumbuka.
16 Na kutakuwa na njia kuu+ kutoka Ashuru kwa ajili ya mabaki+ ya watu wake watakaobaki,+ kama ilivyokuwapo njia kwa ajili ya Israeli siku ile alipokuwa akiondoka katika nchi ya Misri.
8 bali, ‘Yehova yuko hai aliyepandisha na aliyeingiza uzao wa nyumba ya Israeli kutoka katika nchi ya kaskazini na kutoka katika nchi zote ambako nimewatawanya,’ na hakika wao watakaa katika nchi yao wenyewe.”+
17 “Kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya ninyi kutoka katika nchi ambazo katikati yake mmetawanywa, nami nitawapa ninyi udongo wa Israeli.+