Ezekieli
11 Na roho+ ikaniinua juu+ na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yehova linaloelekea mashariki,+ na, tazama! katika mwingilio wa lango kulikuwa na wanaume 25,+ nami nikamwona katikati yao Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, wakuu wa watu.+ 2 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, hawa ndio wanaume wanaopanga hila ya madhara na kutoa mashauri mabaya juu ya jiji hili;+ 3 ambao wanasema, ‘Je, ujenzi wa nyumba haujakaribia?+ Yeye ni chungu cha kupikia chenye mdomo mpana,+ na sisi ni nyama.’
4 “Kwa hiyo toa unabii juu yao. Toa unabii, Ee mwana wa binadamu.”+
5 Ndipo roho ya Yehova ikaniangukia,+ naye akaendelea kuniambia: “Sema, ‘Hivi ndivyo Yehova amesema:+ “Ninyi mlisema jambo lililo sawa, Ee nyumba ya Israeli; na kuhusu mambo yanayokuja katika roho yenu, mimi mwenyewe nimeyajua.+ 6 Mmewafanya waliouawa kati yenu katika jiji hili kuwa wengi, nanyi mmezijaza barabara zake kwa watu waliouawa.” ’ ”+ 7 “Kwa hiyo hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Kuhusu wale waliouawa ambao ninyi mmewaweka katikati yake, wao ni nyama,+ na yeye ndiye chungu cha kupikia chenye mdomo mpana;+ na ninyi wenyewe mtatolewa katikati yake.’ ”+
8 “ ‘Ninyi mmeuogopa upanga,+ nami nitauleta upanga juu yenu,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.+ 9 ‘Nami hakika nitawatoa ninyi katikati yake na kuwatia mkononi mwa wageni+ na kutekeleza juu yenu matendo ya hukumu.+ 10 Kwa upanga mtaanguka.+ Katika mpaka wa Israeli+ nitawahukumu ninyi; nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+ 11 Yeye mwenyewe hatakuwa kwenu chungu cha kupikia chenye mdomo mpana,+ nanyi wenyewe hamtakuwa nyama katikati yake. Katika mpaka wa Israeli nitawahukumu ninyi, 12 nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, kwa sababu hamkutembea katika masharti yangu na hamkuzitenda hukumu zangu,+ bali mmetenda kulingana na hukumu za mataifa yanayowazunguka.’ ”+
13 Na ikawa kwamba mara tu nilipotoa unabii Pelatia mwana wa Benaya mwenyewe akafa,+ nami nikaanguka kifudifudi, nikalia kwa sauti kubwa+ na kusema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova!+ Je, utaangamiza mabaki ya Israeli?”+
14 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 15 “Mwana wa binadamu, kuhusu ndugu zako,+ ndugu zako, wanaume wanaohangaikia haki yako ya kukomboa, na nyumba yote ya Israeli, yote kabisa, ndio ambao wakaaji wa Yerusalemu wamewaambia, ‘Nendeni mbali kutoka kwa Yehova. Ni yetu; tumepewa nchi tuimiliki’;+ 16 kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Ijapokuwa nimewaweka mbali kabisa katikati ya mataifa, na ijapokuwa nimewatawanya katikati ya nchi+ hizo, hata hivyo nitakuwa patakatifu kwao kwa kitambo kidogo katikati ya nchi ambazo wameenda.” ’+
17 “Kwa hiyo sema, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Pia nitawakusanya ninyi kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya ninyi kutoka katika nchi ambazo katikati yake mmetawanywa, nami nitawapa ninyi udongo wa Israeli.+ 18 Nao hakika watakuja huko na kuondoa machukizo yake yote na vinyaa vyake vyote kutoka ndani yake.+ 19 Nami nitawapa moyo mmoja,+ nami nitaweka roho mpya ndani yao;+ nami hakika nitauondoa ule moyo wa jiwe kutoka katika mwili+ wao na kuwapa moyo wa nyama,+ 20 ili watembee katika sheria zangu na kushika maamuzi yangu ya hukumu na kuyatenda;+ na ili wawe watu wangu kwelikweli+ na ili mimi mwenyewe niwe Mungu wao.” ’+
21 “ ‘ “Lakini kwa wale ambao moyo wao unatembea katika machukizo yao na vinyaa vyao,+ hakika nitaleta njia yao wenyewe juu ya vichwa vyao,” asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.’ ”+
22 Na sasa wale makerubi+ wakayainua mabawa yao, na yale magurudumu yalikuwa karibu nao,+ nao utukufu+ wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao, kutoka juu.+ 23 Nao utukufu wa Yehova+ ukapaa kutoka juu katikati ya jiji na kuanza kusimama juu ya mlima+ ulio upande wa mashariki wa jiji hilo.+ 24 Na roho+ ikaniinua+ na mwishowe ikanileta Ukaldayo kwa watu waliohamishwa,+ katika maono kwa roho ya Mungu; na yale maono niliyokuwa nimeyaona yakapaa kutoka juu yangu. 25 Nami nikaanza kuwaambia watu waliohamishwa mambo yote ya Yehova ambayo alikuwa amenifanya niyaone.+