3 ndipo Yehova Mungu wako atakaporudisha mateka+ wako pia na kukuonyesha rehema+ na kukukusanya tena kutoka kwa vikundi vyote vya watu ambako Yehova Mungu wako amekutawanya.+
3 “Nami nitakusanya mabaki ya kondoo zangu kutoka katika nchi zote ambako nilikuwa nimewatawanya,+ nami nitawarudisha kwenye uwanja wao wa malisho,+ na hakika wao watazaa na kuwa wengi.+
13 Nami nitawatoa+ kutoka kwa vikundi vya watu na kuwakusanya pamoja kutoka katika zile nchi na kuwaleta kwenye nchi yao+ na kuwalisha kwenye milima ya Israeli, kando ya vijito na kando ya makao yote ya nchi.+
21 “Nawe uwaambie, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Tazama, ninawachukua wana wa Israeli kutoka katikati ya mataifa ambako wameenda, nami nitawakusanya kutoka pande zote na kuwaleta katika nchi yao.+
11 Na wana wa Yuda na wana wa Israeli hakika watakusanywa pamoja katika umoja+ nao kwa kweli watajiwekea kichwa kimoja nao watatoka katika ile nchi,+ kwa maana siku ya Yezreeli+ itakuwa kuu.