12 Naye hakika atainua ishara kwa ajili ya mataifa na kukusanya watu wa Israeli waliotawanywa;+ na watu wa Yuda waliotawanywa atawakusanya pamoja kutoka miisho minne ya dunia.+
18 “Katika siku hizo watatembea, nyumba ya Yuda ikiwa kando ya nyumba ya Israeli,+ nao pamoja+ watatoka katika nchi ya kaskazini na kuingia katika nchi ambayo niliwapa mababu zenu kuwa fungu la urithi.+
3 Kwa maana, “tazama! siku zinakuja,” asema Yehova, “nami nitawakusanya mateka wa watu wangu, Israeli na Yuda,”+ Yehova amesema, “nami nitawarudisha katika nchi niliyowapa mababu zao, nao hakika wataimiliki tena.”’”+
12 “ ‘Hakika nitamkusanya Yakobo, ninyi nyote;+ bila shaka nitawakusanya pamoja wanaobaki wa Israeli.+ Nitawaunganisha, kama kundi zizini, kama kundi la wanyama katikati ya malisho yake;+ huko kutakuwa na kelele za wanadamu.’+
26 na kwa namna hii Israeli+ wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atatoka katika Sayuni+ na kuondolea mbali mazoea ya kutomwogopa Mungu kutoka katika Yakobo.+