Waroma
11 Basi, nauliza, Je, Mungu aliwakataa watu wake?+ Hilo lisitendeke kamwe! Kwa maana mimi pia ni Mwisraeli,+ wa uzao wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.+ 2 Mungu hakuwakataa watu wake, aliowatambua kwanza.+ Je, hamjui linavyosema Andiko kumhusu Eliya, anapomwomba Mungu dhidi ya Israeli?+ 3 “Yehova, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami peke yangu nimebaki, nao wanaitafuta nafsi yangu.”+ 4 Lakini, neno la Mungu+ linamwambia nini? “Nimebakiza watu elfu saba kwa ajili yangu mwenyewe, watu ambao hawakumpigia Baali goti.”+ 5 Basi, kwa njia hiyo katika majira ya sasa kumetokea pia mabaki+ kulingana na kuchaguliwa+ ambako kunatokana na fadhili zisizostahiliwa. 6 Basi ikiwa ni kwa fadhili zisizostahiliwa,+ si kwa sababu ya matendo+ tena; kama sivyo, fadhili zisizostahiliwa haziwi tena fadhili zisizostahiliwa.+
7 Tuseme nini, basi? Jambo lilelile ambalo Israeli anatafuta kwa bidii yeye hakulipata,+ lakini wale waliochaguliwa+ walilipata. Wale wengine hisia zao zilifanywa kuwa nzito;+ 8 kama ilivyoandikwa: “Mungu amewapa roho ya usingizi mzito,+ macho ili wasione na masikio ili wasisikie, mpaka leo hii.”+ 9 Pia, Daudi anasema: “Meza yao na iwe kwao mnaso na mtego na kikwazo na malipo;+ 10 macho yao na yatiwe giza ili yasione, na sikuzote wauinamishe mgongo wao.”+
11 Kwa hiyo nauliza, Je, walijikwaa hivi kwamba wakaanguka+ kabisa? Hilo lisitendeke kamwe! Lakini kwa kujikwaa+ kwao kuna wokovu kwa watu wa mataifa,+ kuwachochea wao kuwa na wivu.+ 12 Sasa ikiwa kujikwaa kwao humaanisha utajiri kwa ulimwengu, na kupungua kwao humaanisha utajiri kwa watu wa mataifa,+ hesabu+ yao kamili itamaanisha hivyo hata zaidi!
13 Sasa nasema nanyi mlio watu wa mataifa. Kwa maana kama nilivyo, kwa kweli, mtume+ kwa mataifa,+ naitukuza+ huduma+ yangu, 14 ili labda kwa njia yoyote ile niwachochee kuwa na wivu wale ambao ni mwili wangu mwenyewe na kuokoa+ baadhi yao kutoka katikati yao.+ 15 Kwa maana ikiwa kutupwa kwao+ humaanisha upatanisho+ kwa ulimwengu, kupokewa kwao kutamaanisha nini isipokuwa uzima kutoka kwa wafu? 16 Zaidi, ikiwa sehemu inayochukuliwa kuwa matunda ya kwanza+ ni takatifu, donge liko hivyo pia; na ikiwa mzizi ni mtakatifu,+ matawi yako hivyo pia.
17 Hata hivyo, ikiwa matawi mengine yalikatwa lakini wewe, ujapokuwa mzeituni wa mwitu, ulipandikizwa katikati yake+ na kuwa mshiriki wa mzizi wa unono+ wa mzeituni,+ 18 usiwe ukifurahi juu ya hayo matawi. Ingawa hivyo, ikiwa unafurahi juu yake,+ si wewe unayeuchukua mzizi,+ bali ni mzizi unaokuchukua wewe.+ 19 Basi, wewe utasema: “Matawi yalikatwa+ ili mimi nipandikizwe.”+ 20 Vema! Kwa sababu ya ukosefu wao wa imani+ yalikatwa, lakini wewe umesimama kwa imani.+ Uache kuwa na mawazo ya kujivuna,+ bali uogope.+ 21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachilia matawi ya asili, vivyo hivyo hatakuacha wewe.+ 22 Kwa hiyo, ona fadhili+ na ukali+ wa Mungu. Kuna ukali kuwaelekea wale walioanguka,+ lakini kuna fadhili za Mungu kukuelekea wewe, ila tu ukae+ katika fadhili zake; kama sivyo, wewe pia utakatwa.+ 23 Wao pia, ikiwa hawatadumu katika ukosefu wao wa imani, watapandikizwa;+ kwa maana Mungu anaweza kuwapandikiza tena. 24 Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa kutoka kwenye mzeituni ulio wa asili ya mwituni na kupandikizwa+ kinyume cha asili katika mzeituni wa bustanini, si afadhali zaidi kwamba hawa walio wa asili wapandikizwe katika mzeituni wao wenyewe!+
25 Kwa maana sitaki ninyi, akina ndugu, mkose kuijua siri hii takatifu,+ kusudi msiwe wenye busara machoni penu wenyewe: kwamba, kwa sehemu, kumekuwa na kutiwa uzito kwa hisi+ za Israeli mpaka hesabu+ kamili ya watu wa mataifa iwe imeingia,+ 26 na kwa namna hii Israeli+ wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atatoka katika Sayuni+ na kuondolea mbali mazoea ya kutomwogopa Mungu kutoka katika Yakobo.+ 27 Na hili ndilo agano kwa upande wangu pamoja nao,+ nitakapoondolea mbali dhambi zao.”+ 28 Ni kweli, kuhusiana na habari njema wao ni adui kwa ajili yenu,+ lakini kuhusiana na kuchagua kwa Mungu wao ni wapendwa kwa ajili ya mababu zao.+ 29 Kwa maana zawadi na mwito wa Mungu si mambo ambayo yeye atajutia.+ 30 Kwa maana kama vile ninyi wakati mmoja mlivyokuwa hamtii+ Mungu lakini sasa mmeonyeshwa rehema+ kwa sababu ya kutotii kwao,+ 31 ndivyo pia hawa sasa wamekuwa wasiotii ikitokeza rehema kwenu,+ ili wao wenyewe pia waonyeshwe rehema sasa. 32 Kwa maana Mungu amewafunga wote pamoja katika kutotii,+ ili awaonyeshe wao wote rehema.+
33 Lo! Jinsi kilivyo kina cha utajiri+ wa Mungu na hekima+ na ujuzi!+ Jinsi hukumu+ zake zisivyochunguzika na njia zake zisivyotafutika! 34 Kwa maana “ni nani amekuja kuijua akili+ ya Yehova, au ni nani amekuwa mshauri wake?”+ 35 Au, “Ni nani amempa yeye kwanza, hivi kwamba iwe lazima arudishiwe?”+ 36 Kwa sababu vitu vyote ni kutoka kwake na kwa yeye na kwa ajili yake.+ Kwake yeye na kuwe na utukufu milele.+ Amina.