Isaya
43 Na sasa Yehova, Muumba+ wako, Ee Yakobo, na Mfanyizaji+ wako, Ee Israeli, amesema hivi: “Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+ Nimekuita kwa jina lako.+ Wewe ni wangu.+ 2 Ukipita katikati ya maji,+ nitakuwa pamoja nawe;+ na katikati ya mito, haitafurika juu yako.+ Ukitembea katikati ya moto, hutaungua, wala mwali wa moto hautakuchoma.+ 3 Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wako, Mtakatifu wa Israeli Mwokozi wako.+ Nimetoa Misri kuwa fidia kwa ajili yako,+ Ethiopia+ na Seba badala yako. 4 Kwa sababu umekuwa mwenye thamani machoni pangu,+ umeonwa kuwa mwenye kuheshimika, na mimi mwenyewe nimekupenda.+ Nami nitawatoa watu badala yako, na vikundi vya mataifa badala ya nafsi yako.+
5 “Usiogope, kwa maana nipo pamoja nawe.+ Kutoka mashariki nitauleta uzao wako, nami nitakukusanya pamoja kutoka magharibi.+ 6 Nitaiambia kaskazini,+ ‘Toa!’ na kusini, ‘Usizuie. Walete wanangu kutoka mbali, na binti zangu kutoka mwisho wa dunia,+ 7 kila mtu ambaye anaitwa kwa jina langu+ na ambaye nimemuumba kwa ajili ya utukufu wangu,+ ambaye nimemfanya, ndiyo, ambaye nimemfanyiza.’+
8 “Leteni kikundi cha watu ambao ni vipofu ingawa macho yapo, na walio viziwi ingawa wana masikio.+ 9 Mataifa yote na yakusanywe mahali pamoja, na vikundi vya mataifa vikusanywe pamoja.+ Ni nani kati yao anayeweza kutangaza haya?+ Au, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza?+ Na watoe mashahidi wao,+ ili watangazwe kuwa waadilifu, au wasikie na kusema, ‘Ni kweli!’”+
10 “Ninyi ni mashahidi wangu,”+ asema Yehova, “mtumishi wangu ambaye nimemchagua,+ ili mjue+ na kuwa na imani katika mimi,+ na ili mwelewe kwamba mimi ni Yeye yuleyule.+ Kabla yangu hakuna Mungu yeyote aliyefanyizwa,+ na baada yangu hapakuendelea kuwapo yeyote.+ 11 Mimi—mimi ni Yehova,+ na zaidi ya mimi hakuna mwokozi.”+
12 “Mimi mwenyewe nimetangaza na kuokoa na kufanya lisikiwe,+ wakati hapakuwa na mungu yeyote mgeni katikati yenu.+ Basi ninyi ni mashahidi wangu,”+ asema Yehova, “nami ni Mungu.+ 13 Pia, wakati wote mimi ni Yeye yuleyule;+ na hakuna yeyote anayekomboa kutoka katika mkono wangu.+ Nitatenda,+ na ni nani anayeweza kuurudisha nyuma?”+
14 Yehova, Mkombozi wenu,+ Mtakatifu wa Israeli,+ amesema hivi: “Nitatuma ujumbe huko Babiloni kwa ajili yenu na kuyashusha mapingo ya magereza,+ na Wakaldayo katika meli kwa vilio vyao vya kulalamika.+ 15 Mimi ni Yehova Mtakatifu wenu,+ Muumba wa Israeli,+ Mfalme wenu.”+
16 Amesema hivi Yehova, Yeye anayefanya njia katikati ya bahari na barabara katikati ya maji yenye nguvu,+ 17 Yeye anayetoa gari la vita na farasi, jeshi na wenye nguvu wakati uleule:+ “Watalala chini.+ Hawataamka.+ Hakika watazimwa.+ Watazimwa kama utambi wa kitani.”+
18 “Msiyakumbuke yale mambo ya kwanza, wala msiyafikirie yale mambo ya zamani. 19 Tazama! Ninafanya jambo jipya.+ Sasa litachipuka. Ninyi mtalijua, sivyo?+ Kwa kweli, nitaweka njia kupitia nyikani,+ kupitia mito ya jangwani.+ 20 Mnyama wa mwituni atanitukuza,+ mbwa-mwitu na mbuni;+ kwa sababu nitakuwa nimewapa maji hata katika nyika, mito katika jangwa,+ ili kuwafanya watu wangu, mchaguliwa wangu,+ wanywe, 21 watu ambao nimejifanyia, ili wasimulie sifa zangu.+
22 “Lakini wewe hukuniita mimi, Ee Yakobo,+ kwa sababu umechoka nami, Ee Israeli.+ 23 Hukuniletea kondoo wa matoleo yako mazima ya kuteketezwa, wala hukunitukuza kwa dhabihu zako.+ Mimi sikukulazimisha unitumikie na zawadi, wala sikukuchosha na ubani.+ 24 Hukuninunulia kwa pesa yoyote kane tamu;+ wala hukunijaza mimi kwa mafuta ya dhabihu zako.+ Kwa kweli umenilazimisha kutumikia kwa sababu ya dhambi zako; umenichosha kwa makosa yako.+
25 “Mimi—mimi ndiye Yeye anayefuta+ makosa+ yako kwa ajili yangu mwenyewe,+ na dhambi zako sitazikumbuka.+ 26 Nikumbushe; na tujiweke hukumuni pamoja;+ toa masimulizi yako kuhusu jambo hilo ili uwe upande wa haki.+ 27 Baba yako, yule wa kwanza, ametenda dhambi,+ na wasemaji wako wamenikosea.+ 28 Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa mahali patakatifu, nami nitamtoa Yakobo awe mtu wa kuangamizwa na kumtoa Israeli kwa ajili ya matukano.+