Ezekieli
20 Ikawa kwamba katika mwaka wa saba, katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi huo, baadhi ya watu kati ya wazee wa Israeli wakaja kuuliza juu ya Yehova,+ nao wakaketi mbele yangu.+ 2 Ndipo neno la Yehova likanijia, na kusema: 3 “Mwana wa binadamu, sema na wanaume wazee wa Israeli, nawe utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Je, mnakuja kuuliza neno juu yangu?+ ‘Kama ninavyoishi, hamtauliza neno juu yangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” ’
4 “Je, utawahukumu? Je, utawahukumu, Ee mwana wa binadamu?+ Wajulishe machukizo ya mababu zao.+ 5 Nawe utawaambia, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Katika siku ile nilipochagua Israeli,+ pia niliuinua mkono+ wangu katika kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo+ na kujijulisha kwao katika nchi ya Misri.+ Naam, niliuinua mkono wangu katika kiapo kwao, na kusema, ‘Mimi ni Yehova Mungu wenu.’+ 6 Katika siku hiyo niliuinua mkono+ katika kiapo kwao ili kuwatoa katika nchi ya Misri mpaka katika nchi niliyokuwa nimeipeleleza kwa ajili yao, yenye kutiririka maziwa na asali.+ Hiyo ilikuwa ni pambo la nchi zote.+ 7 Nami nikaendelea kuwaambia, ‘Tupilieni mbali, kila mmoja wenu, machukizo ya macho yake,+ nanyi msijitie unajisi kwa sanamu za mavi za Misri.+ Mimi ni Yehova Mungu wenu.’+
8 “ ‘ “Nao wakaanza kuniasi,+ wala hawakukubali kunisikiliza. Kila mmoja wao hakuyatupilia mbali machukizo ya macho yake, nazo sanamu zao za mavi za Misri hawakuziacha,+ hivi kwamba nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiliza hasira yangu juu yao katikati ya nchi ya Misri.+ 9 Nami nikachukua hatua kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa ambayo walikuwa katikati yao,+ kwa sababu nilikuwa nimejijulisha kwao mbele ya macho yao kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.+ 10 Kwa hiyo nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaingiza nyikani.+
11 “ ‘ “Nami nikawapa sheria+ zangu; nayo maamuzi yangu ya hukumu+ nikawajulisha, ili mtu ambaye huendelea kuyafanya aweze pia kuishi kwa hayo.+ 12 Nami nikawapa pia sabato zangu,+ ziwe ishara kati yangu nao,+ ili wajue kwamba mimi ni Yehova ninayewatakasa.
13 “ ‘ “Lakini wao, nyumba ya Israeli, waliniasi nyikani.+ Hawakutembea katika sheria+ zangu, nao wakayakataa maamuzi yangu ya hukumu,+ ambayo, mtu akiendelea kuyafanya, pia ataendelea kuishi kwa hayo.+ Nazo sabato zangu walizitia unajisi sana,+ hivi kwamba nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao nyikani, ili kuwaangamiza.+ 14 Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu mwenyewe ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao nilikuwa nimewatoa mbele ya macho yao.+ 15 Na mimi mwenyewe pia nikawainulia mkono wangu katika kiapo nyikani,+ kwamba sitawaingiza katika nchi niliyokuwa nimeitoa, yenye kutiririka maziwa na asali,+ (hiyo ni pambo la nchi zote,)+ 16 kwa sababu walikataa maamuzi yangu mwenyewe ya hukumu; nazo sheria zangu, hawakutembea katika hizo, nazo sabato zangu walizitia unajisi, kwa sababu moyo wao ulikuwa ukifuatilia sanamu zao za mavi.+
17 “ ‘ “Nalo jicho langu likaanza kuwasikitikia ili kunizuia nisiwaharibu,+ nami sikuwaangamiza nyikani. 18 Nami nikawaambia wana wao nyikani,+ ‘Msitembee katika masharti ya mababu zenu,+ wala msizishike hukumu zao,+ wala msijitie unajisi kwa sanamu zao za mavi.+ 19 Mimi ni Yehova Mungu wenu.+ Tembeeni katika sheria+ zangu mwenyewe, na kuyashika maamuzi yangu mwenyewe ya hukumu+ na kuyafanya.+ 20 Na zitakaseni sabato zangu mwenyewe,+ nazo zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, ili mjue kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’+
21 “ ‘ “Na hao wana wakaanza kuniasi.+ Hawakutembea katika sheria zangu, nayo maamuzi yangu ya hukumu hawakuendelea kuyashika kwa kuyafanya, ambayo, kama mtu akiendelea kuyafanya, ataendelea pia kuishi kwa hayo.+ Sabato zangu walizitia unajisi.+ Kwa hiyo nikaahidi kumwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiliza hasira yangu juu yao nyikani.+ 22 Nami nikaurudisha mkono wangu+ na kutenda kwa ajili ya jina langu mwenyewe, ili lisitiwe unajisi mbele ya macho ya mataifa, ambao nilikuwa nimewatoa mbele ya macho yao.+ 23 Pia, mimi mwenyewe niliwainulia mkono wangu katika kiapo nyikani,+ ili kuwatawanya kati ya mataifa na kuwatawanya kati ya nchi mbalimbali,+ 24 kwa sababu hawakufanya maamuzi yangu mwenyewe ya hukumu+ nao walizikataa sheria zangu mwenyewe+ nao wakazitia unajisi sabato zangu mwenyewe,+ nayo macho yao yalizifuata sanamu za mavi za mababu zao.+ 25 Na mimi mwenyewe pia niliwaacha wawe na masharti ambayo hayakuwa mazuri na maamuzi ya hukumu ambayo hawangeweza kuendelea kuishi kulingana nayo.+ 26 Nami nikawa nikiwaacha watiwe unajisi kwa zawadi zao walipomfanya kila mtoto aliyelifungua tumbo la uzazi apite katikati ya moto,+ ili niwafanye ukiwa, ili wapate kujua kwamba mimi ni Yehova.” ’+
27 “Kwa hiyo sema na nyumba ya Israeli, Ee mwana wa binadamu, nawe utawaambia hivi,+ ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Hata katika habari hii, mababu zenu walisema vibaya juu yangu, kwa kunitendea kwa ukosefu wa uaminifu.+ 28 Nami nikawaleta katika nchi+ ambayo nilikuwa nimeuinua mkono wangu katika kiapo kwamba nitawapa wao.+ Walipoona kila kilima kilichoinuka+ na kila mti wenye matawi mengi, ndipo wakaanza kutoa dhabihu+ zao huko na kutolea huko matoleo yao yenye kuudhi, na kutolea huko harufu zao za kutuliza+ na kumimina huko matoleo yao ya kinywaji.+ 29 Kwa hiyo nikawaambia, ‘Mahali pa juu mnapokuja panamaanisha nini, hivi kwamba paitwe jina lake Mahali pa Juu mpaka leo hii?’ ” ’+
30 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Je, ninyi mnajitia unajisi katika njia za mababu zenu,+ na je, katika kufuatilia machukizo yao mnaingilia kufanya uasherati?+ 31 Na katika kuinua zawadi zenu kwa kuwafanya wana wenu wapite katikati ya moto,+ je, mnajitia unajisi kwa ajili ya sanamu zenu zote za mavi mpaka leo hii?+ Wakati huohuo je, mtauliza neno juu yangu, Ee nyumba ya Israeli?” ’+
“ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘Hamtauliza juu yangu.+ 32 Na kile kinachoingia katika roho yenu+ hakika hakitatukia,+ kwa kuwa mnasema: “Na tuwe kama mataifa, kama familia za nchi mbalimbali,+ katika kuhudumia miti na mawe.” ’ ”+
33 “ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘nitatawala nikiwa mfalme juu yenu kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa+ na kwa ghadhabu iliyomwagwa.+ 34 Nami nitawatoa kati ya vikundi vya watu, nami nitawakusanya pamoja kutoka katika nchi ambako mmetawanywa kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa na kwa ghadhabu iliyomwagwa.+ 35 Nami nitawaleta katika nyika ya vikundi vya watu+ na kujiweka katika hukumu pamoja nanyi huko uso kwa uso.+
36 “ ‘Kama vile nilivyojiweka mwenyewe katika hukumu pamoja na mababu zenu katika nyika ya nchi ya Misri,+ ndivyo nitakavyojiweka mwenyewe katika hukumu pamoja nanyi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova. 37 ‘Nami nitawafanya mpite chini ya fimbo+ na kuwaingiza katika kifungo cha agano.+ 38 Nami nitasafishia mbali kutoka kwenu wale wanaoasi na wale wanaonikosea,+ kwa maana kutoka katika nchi ya makao yao ya kigeni nitawaleta, lakini hawatakuja kwenye udongo wa Israeli;+ nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+
39 “Nanyi, Ee nyumba ya Israeli, hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema, ‘Nendeni kila mmoja wenu akazitumikie sanamu zake mwenyewe za mavi.+ Na baadaye ikiwa hamnisikilizi, basi hamtaendelea kulitia unajisi jina langu takatifu kwa zawadi zenu na kwa sanamu zenu za mavi.’+
40 “ ‘Kwa maana katika mlima wangu mtakatifu, katika mlima wa kilele cha Israeli,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, ‘huko ndiko wao, nyumba yote ya Israeli ikiwa nzima, itanitumikia, katika nchi ile.+ Nitafurahishwa nao huko, na huko nitaitaka michango yenu na matunda ya kwanza ya matoleo yenu katika vitu vyenu vyote vilivyo vitakatifu.+ 41 Kwa sababu ya harufu ya kutuliza nitafurahishwa nanyi,+ nitakapowatoa kati ya vikundi vya watu nami hakika niwakusanye pamoja kutoka katika nchi ambazo mmetawanywa,+ nami nitatakaswa ndani yenu mbele ya macho ya mataifa.’+
42 “ ‘Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ nitakapowaleta kwenye udongo wa Israeli,+ katika nchi ambayo niliuinua mkono wangu katika kiapo kwamba nitawapa mababu zenu. 43 Nanyi hakika mtakumbuka huko njia zenu na matendo yenu yote+ ambayo mlijitia unajisi kwa hayo,+ nanyi hakika mtajichukia mbele ya nyuso zenu wenyewe kwa sababu ya mambo yenu yote mabaya ambayo mliyatenda.+ 44 Nanyi mtalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova+ nitakapochukua hatua kuhusiana nanyi kwa ajili ya jina langu,+ si kulingana na njia zenu mbaya au kulingana na matendo yenu yenye uharibifu,+ Ee nyumba ya Israeli,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
45 Nalo neno la Yehova likaendelea kunijia, na kusema: 46 “Mwana wa binadamu, elekeza uso+ wako upande wa eneo la kusini na udondoshe+ maneno kuelekea kusini, na utoe unabii kwa msitu wa uwanja wa kusini. 47 Nawe utauambia msitu wa kusini, ‘Sikia neno la Yehova. Hivi ndivyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema: “Tazama, ninawasha moto juu yako,+ nao utateketeza ndani yako kila mti ambao ungali mbichi na kila mti uliokauka.+ Mwali huo wa moto unaowaka hautazimwa,+ na kwa huo nyuso zote zitateketezwa kutoka kusini mpaka kaskazini.+ 48 Na watu wote wenye mwili wataona kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimeuwasha moto, ili usipate kuzimwa.” ’ ”+
49 Nami nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Wanasema juu yangu, ‘Je, yeye hatungi maneno ya kimethali?’ ”+