9 Nao manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu. Mifupa yangu yote imeanza kutetemeka. Nimekuwa kama mtu ambaye amelewa,+ na kama mwanamume ambaye divai imemlemea, kwa sababu ya Yehova na kwa sababu ya maneno yake matakatifu.
27 Na mimi, Danieli, nikachoka kabisa, nikawa mgonjwa kwa muda wa siku fulani.+ Kisha nikaamka na kufanya kazi ya mfalme;+ lakini nikaendelea kuonekana nimekufa ganzi kwa sababu ya lile jambo lililoonwa, wala hakuna mtu aliyelielewa.+