א [ʼAʹleph]
119 Wenye furaha ni wale wasio na kosa katika njia yao,+
Wale wanaotembea katika sheria ya Yehova.+
2 Wenye furaha ni wale wanaoshika vikumbusho vyake;+
Wanaendelea kumtafuta kwa moyo wote.+
3 Kwa kweli hawakuzoea kufanya ukosefu wowote wa uadilifu.+
Wametembea katika njia zake.+
4 Wewe mwenyewe umetoa maagizo yako kwa kuamuru+
Yashikwe kwa uangalifu.+
5 Laiti njia zangu zingefanywa imara+
Ili kushika masharti yako!+
6 Ndipo singeona aibu,+
Ninapozitazama amri zako zote.+
7 Nitakusifu katika unyoofu wa moyo,+
Ninapojifunza maamuzi yako ya hukumu yaliyo ya uadilifu.+
8 Ninaendelea kushika masharti yako.+
Ee, usiniache kabisa.+
ב [Behth]
9 Kijana+ ataisafishaje njia yake?
Kwa kujilinda kulingana na neno lako.+
10 Nimekutafuta kwa moyo wangu wote.+
Usinipotoshe niache amri zako.+
11 Moyoni mwangu nimeweka hazina ya maneno yako,+
Ili nisikutendee dhambi.+
12 Umebarikiwa, Ee Yehova.
Unifundishe masharti yako.+
13 Kwa midomo yangu nimetangaza+
Maamuzi yote ya hukumu ya kinywa chako.+
14 Nimeshangilia katika njia ya vikumbusho vyako,+
Kama vile katika mambo mengine yote yenye thamani.+
15 Nitajishughulisha na maagizo yako,+
Nami nitayatazama mapito yako.+
16 Nitazipenda sheria zako.+
Sitalisahau neno lako.+
ג [Giʹmel]
17 Umtendee mtumishi wako inavyofaa, ili nipate kuishi+
Na ili nipate kulishika neno lako.+
18 Ufunue macho yangu, ili nipate kutazama+
Mambo ya ajabu kutoka katika sheria yako.+
19 Mimi ni mkaaji mgeni tu katika nchi.+
Usinifiche amri zako.+
20 Nafsi yangu imepondeka kwa kutamani+
Maamuzi yako ya hukumu wakati wote.+
21 Umewakemea wenye kimbelembele waliolaaniwa,+
Ambao wanaziacha amri zako.+
22 Niondolee shutuma na dharau,+
Kwa maana nimeshika vikumbusho vyako.+
23 Hata wakuu wameketi; Wamesemezana dhidi yangu.+
Naye mtumishi wako, anajishughulisha na masharti yako.+
24 Pia, ninavipenda vikumbusho vyako,+
Ni kama wanaume wa shauri langu.+
ד [Daʹleth]
25 Nafsi yangu imekuwa ikishikamana na mavumbi.+
Nihifadhi hai kulingana na neno lako.+
26 Nimezitangaza njia zangu mwenyewe, ili unijibu.+
Unifundishe masharti yako.+
27 Unifanye nielewe njia ya maagizo yako mwenyewe,+
Ili nipate kujishughulisha na kazi zako za ajabu.+
28 Nafsi yangu imekosa usingizi kwa sababu ya huzuni.+
Uniinue kulingana na neno lako.+
29 Uniondolee njia ya uwongo,+
Na kunipa kibali kwa sheria yako.+
30 Nimeichagua njia ya uaminifu.+
Nimeyaona maamuzi yako ya hukumu kuwa yenye kufaa.+
31 Nimeshikamana na vikumbusho vyako.+
Ee Yehova, usiniaibishe.+
32 Nitakimbia kwenye njia ya amri zako,+
Kwa sababu wewe huufanya moyo wangu upate nafasi.+
ה [Heʼ]
33 Unifundishe, Ee Yehova, njia ya masharti yako,+
Ili nipate kuishika hata ile ya mwisho.+
34 Unifanye nielewe, ili nipate kuishika sheria yako+
Nami nipate kuishika kwa moyo wote.+
35 Unitembeze katika njia ya amri zako,+
Kwa maana nimependezwa nayo.+
36 Uelekeze moyo wangu kwa vikumbusho vyako,+
Wala si kwa faida.+
37 Uyafanye macho yangu yapite ili yasione jambo lisilofaa;+
Unihifadhi hai katika njia yako mwenyewe.+
38 Umtimizie mtumishi wako maneno yako+
Ambayo yanamwelekeza kukuogopa wewe.+
39 Ufanye shutuma yangu ipitilie mbali, ambayo nimeiogopa,+
Kwa maana maamuzi yako ya hukumu ni mema.+
40 Tazama! nimeyatamani maagizo yako.+
Unihifadhi hai katika uadilifu wako.+
ו [Waw]
41 Na fadhili zako zenye upendo na zinijie, Ee Yehova,+
Wokovu wako kulingana na maneno yako,+
42 Nipate kumjibu yeye anayenishutumu kwa neno,+
Kwa maana nimelitegemea neno lako.+
43 Wala usiondoe kabisa neno la kweli kutoka kinywani mwangu,+
Kwa maana nimengojea uamuzi wako mwenyewe wa hukumu.+
44 Nami nitaishika sheria yako daima,+
Mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
45 Nami nitatembea huku na huku katika mahali penye nafasi tele,+
Kwa maana nimeyatafuta maagizo yako.+
46 Pia nitasema juu ya vikumbusho vyako mbele ya wafalme,+
Wala sitaona aibu.+
47 Nami nitapendezwa na amri zako+
Ambazo nimezipenda.+
48 Nami nitainua mikono yangu kwenye amri zako ambazo nimezipenda,+
Nami nitajishughulisha mwenyewe na masharti yako.+
ז [Zaʹyin]
49 Ulikumbuke neno lako kwa mtumishi wako,+
Ambalo umenifanya nilingojee.+
50 Hii ndiyo faraja yangu katika mateso yangu,+
Kwa maana maneno yako mwenyewe yamenihifadhi hai.+
51 Wenye kimbelembele wamenidharau kupindukia.+
Sijageuka kando kutoka kwenye sheria yako.+
52 Nimeyakumbuka maamuzi yako ya hukumu tangu wakati usio na kipimo, Ee Yehova,+
Nami najipatia faraja.+
53 Hasira inayowaka imenishika kwa sababu ya waovu,+
Wanaoiacha sheria yako.+
54 Masharti yako yamekuwa muziki kwangu+
Katika nyumba ya makao yangu ya kigeni.+
55 Nimekumbuka jina lako usiku, Ee Yehova,+
Ili nipate kuishika sheria yako.+
56 Yote hayo yamekuwa yangu,
Kwa sababu nimeyashika maagizo yako.+
ח [Chehth]
57 Yehova ni fungu langu;+
Nimeahidi kuyashika maneno yako.+
58 Nimeutuliza uso wako kwa moyo wangu wote.+
Unionyeshe kibali kulingana na maneno yako.+
59 Nimezifikiria njia zangu,+
Ili nipate kuirudisha miguu yangu kwenye vikumbusho vyako.+
60 Nilifanya haraka, nami sikukawia+
Kuzishika amri zako.+
61 Kamba za waovu zilinizingira.+
Sikuisahau sheria yako.+
62 Katikati ya usiku mimi huamka ili kukushukuru+
Kwa ajili ya maamuzi yako ya hukumu ya uadilifu.+
63 Mimi ni mwenzao watu wote wanaokuogopa wewe,+
Na wale wanaoyashika maagizo yako.+
64 Fadhili zako zenye upendo, Ee Yehova, zimeijaza dunia.+
Unifundishe masharti yako mwenyewe.+
ט [Tehth]
65 Umemtendea mtumishi wako vema,+
Ee Yehova, kulingana na neno lako.+
66 Unifundishe wema,+ kuwa na akili+ na ujuzi,+
Kwa maana nimeonyesha imani katika amri zako.+
67 Kabla ya kuteseka nilikuwa nikifanya dhambi bila kukusudia,+
Bali sasa nimelishika neno lako.+
68 Wewe ni mwema nawe unatenda mema.+
Unifundishe masharti yako.+
69 Wenye kimbelembele wamenipaka uwongo.+
Bali mimi, nitayashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.+
70 Moyo wao umekosa hisia kama mafuta.+
Mimi nami, nimependezwa na sheria yako.+
71 Ni vema kwamba nimeteseka,+
Ili nipate kujifunza masharti yako.+
72 Sheria+ ya kinywa chako ni njema kwangu,+
Kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha.+
י [Yohdh]
73 Mikono yako mwenyewe imenifanya, nayo ikaniweka imara.+
Unifanye nielewe, ili nipate kujifunza amri zako.+
74 Wale wanaokuogopa ndio wanaoniona na kushangilia,+
Kwa maana nimelingojea neno lako mwenyewe.+
75 Najua vema, Ee Yehova, kwamba maamuzi yako ya hukumu ni uadilifu+
Na kwamba umenitesa kwa uaminifu.+
76 Tafadhali, fadhili zako zenye upendo na zinifariji,+
Kulingana na maneno yako kwa mtumishi wako.+
77 Rehema zako na zinijie, ili nipate kuendelea kuishi;+
Kwa maana sheria yako ndiyo inayonipendeza.+
78 Wenye kimbelembele na waone aibu, kwa maana wamenipotosha bila sababu.+
Bali mimi, najishughulisha na maagizo yako.+
79 Wale wanaokuogopa na warudi kwangu,+
Wale pia wanaovijua vikumbusho vyako.+
80 Moyo wangu uwe hauna kosa katika masharti yako,+
Ili nisione aibu.+
כ [Kaph]
81 Nafsi yangu imedhoofika kwa kutamani wokovu wako;+
Neno lako nimelingojea.+
82 Macho yangu yamedhoofika kwa kutamani maneno yako,+
Huku mimi nikisema: “Utanifariji wakati gani?”+
83 Kwa maana nimekuwa kama kiriba+ katika moshi.
Masharti yako sijayasahau.+
84 Siku za mtumishi wako ni ngapi?+
Utatekeleza hukumu wakati gani juu ya wale wanaonitesa?+
85 Wenye kimbelembele wamechimba mashimo ya mtego ili wanipate,+
Wale ambao hawakubaliani na sheria yako.+
86 Amri zako zote ni uaminifu.+
Wamenitesa bila sababu. Ee unisaidie.+
87 Baada ya muda kidogo wangeniangamiza duniani;+
Bali mimi sikuyaacha maagizo yako.+
88 Unihifadhi hai kulingana na fadhili zako zenye upendo,+
Ili nipate kushika kikumbusho cha kinywa chako.+
ל [Laʹmedh]
89 Mpaka wakati usio na kipimo, Ee Yehova,+
Neno lako limesimama mbinguni.+
90 Uaminifu wako ni wa kizazi baada ya kizazi.+
Umeiweka dunia imara, ili ipate kuendelea kusimama.+
91 Kulingana na maamuzi yako ya hukumu, vimesimama mpaka leo,+
Kwa maana vyote hivyo ni watumishi wako.+
92 Ikiwa singaliipenda sheria yako,+
Basi ningaliangamia katika mateso yangu.+
93 Sitayasahau maagizo yako mpaka wakati usio na kipimo,+
Kwa sababu umenihifadhi hai kupitia hayo.+
94 Mimi ni wako. Uniokoe,+
Kwa sababu nimeyatafuta maagizo yako.+
95 Waovu wameningojea wapate kuniangamiza.+
Nami ninaendelea kuvikazia fikira vikumbusho vyako.+
96 Nimeona mwisho wa ukamilifu wote.+
Amri yako ni pana sana.
מ [Mem]
97 Jinsi ninavyoipenda sheria yako!+
Ndiyo ninayoihangaikia mchana kutwa.+
98 Amri yako hunifanya kuwa na hekima kuliko adui zangu,+
Kwa sababu ni yangu mpaka wakati usio na kipimo.+
99 Nimepata kuwa na ufahamu kuliko walimu wangu wote,+
Kwa sababu vikumbusho vyako ndivyo ninavyohangaikia.+
100 Najiendesha kwa uelewaji mwingi kuliko wanaume wazee,+
Kwa sababu nimeyashika maagizo yako.+
101 Nimeizuilia mbali miguu yangu kutoka katika kila pito baya,+
Kusudi nipate kulishika neno lako.+
102 Sijageuka kando kutoka katika maamuzi yako ya hukumu,+
Kwa maana wewe mwenyewe umenifundisha.+
103 Jinsi maneno yako yamekuwa laini katika kaakaa langu,
Kuliko asali kinywani mwangu!+
104 Ninajiendesha kwa uelewaji kwa sababu ya maagizo yako.+
Ndiyo sababu nimeichukia kila njia ya uwongo.+
נ [Nun]
105 Neno lako ni taa ya mguu wangu,+
Na nuru kwa barabara yangu.+
106 Nimetoa ahadi yenye kiapo, nami nitaitimiza,+
Kuyashika maamuzi yako ya hukumu ya uadilifu.+
107 Nimeteseka kwa kiasi kikubwa.+
Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na neno lako.+
108 Tafadhali furahia matoleo ya hiari ya kinywa changu, Ee Yehova,+
Na unifundishe maamuzi yako ya hukumu.+
109 Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima;+
Lakini sheria yako sijaisahau.+
110 Waovu wamenitegea mtego,+
Lakini sijaondoka katika maagizo yako.+
111 Nimevichukua vikumbusho vyako kuwa ni urithi mpaka wakati usio na kipimo,+
Kwa maana hivyo ni furaha ya moyo wangu.+
112 Nimeuelekeza moyo wangu ili kuyatenda masharti yako+
Mpaka wakati usio na kipimo, mpaka lile la mwisho.+
ס [Saʹmekh]
113 Nimewachukia wenye moyo nusu nusu,+
Lakini sheria yako nimeipenda.+
114 Wewe ni mahali pangu pa kujificha na ngao yangu.+
Kwa maana nimelingojea neno lako.+
115 Ondokeni kwangu, enyi watenda-maovu,+
Ili nipate kuzishika amri za Mungu wangu.+
116 Unitegemeze kulingana na neno lako, ili niendelee kuishi,+
Wala usiniaibishe kwa ajili ya tumaini langu.+
117 Unitegemeze, ili nipate kuokolewa,+
Nami nitayaangalia masharti yako daima.+
118 Umewarusha mbali wale wote wanaoondoka katika masharti yako;+
Kwa maana ujanja wao ni uwongo.+
119 Umewakomesha waovu wote wa dunia kama takataka.+
Kwa hiyo nimevipenda vikumbusho vyako.+
120 Mwili wangu umetetemeka kwa sababu ya kukuhofu;+
Nami nimeogopa kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu.+
ע [ʽAʹyin]
121 Nimetekeleza hukumu na uadilifu.+
Usiniache mikononi mwa wale wanaonipunja!+
122 Uwe mdhamini wa mtumishi wako kwa ajili ya lililo jema.+
Wenye kimbelembele wasinipunje.+
123 Macho yangu yamedhoofika kwa ajili ya wokovu wako+
Na kwa ajili ya neno lako la uadilifu.+
124 Mtendee mtumishi wako kulingana na fadhili zako zenye upendo,+
Na unifundishe masharti yako mwenyewe.+
125 Mimi ni mtumishi wako.+ Nifanye nielewe,+
Ili nipate kuvijua vikumbusho vyako.+
126 Ni wakati wa Yehova kutenda.+
Wameivunja sheria yako.+
127 Ndiyo sababu nimezipenda amri zako+
Kuliko dhahabu, naam, dhahabu safi.+
128 Ndiyo sababu nimeyaona maagizo yote juu ya mambo yote kuwa ni sawa;+
Nimechukia kila njia ya uwongo.+
פ [Peʼ]
129 Vikumbusho vyako ni vizuri ajabu.+
Ndiyo sababu nafsi yangu imevishika.+
130 Kufunuliwa kwa maneno yako hutoa nuru,+
Kukiwafanya wasio na uzoefu waelewe.+
131 Nimekifungua kinywa changu wazi, ili nipate kupumua,+
Kwa sababu nimezitamani amri zako.+
132 Unigeukie na kunionyesha kibali,+
Kulingana na uamuzi wako wa hukumu kuwaelekea wale wanaolipenda jina lako.+
133 Uweke imara hatua zangu katika maneno yako,+
Wala namna yoyote ya jambo lenye kuumiza lisinitawale.+
134 Unikomboe na yeyote anayewapunja wanadamu,+
Nami nitayashika maagizo yako.+
135 Ufanye uso wako umwangazie mtumishi wako,+
Na unifundishe masharti yako.+
136 Vijito vya maji vimetiririka kutoka machoni pangu+
Kwa sababu hawakuishika sheria yako.+
צ [Tsa·dhehʹ]
137 Wewe ni mwadilifu, Ee Yehova,+
Nayo maamuzi yako ya hukumu ni manyoofu.+
138 Umeviamuru vikumbusho+ vyako kwa uadilifu
Na kwa uaminifu mwingi.+
139 Bidii yangu imenimaliza,+
Kwa sababu wapinzani wangu wameyasahau maneno yako.+
140 Neno lako ni safi sana,+
Na mtumishi wako analipenda.+
141 Mimi ni mnyonge na wa kudharaulika.+
Sijayasahau maagizo
yako.+
142 Uadilifu wako ni uadilifu wa mpaka wakati usio na kipimo,+
Na sheria yako ni kweli.+
143 Nilipata taabu na magumu.+
Nilipendezwa na amri zako.+
144 Uadilifu wa vikumbusho vyako ni wa mpaka wakati usio na kipimo.+
Nifanye nielewe, ili nipate kuendelea kuishi.+
ק [Qohph]
145 Nimeita kwa moyo wangu wote.+ Unijibu, Ee Yehova.+
Nitayashika masharti yako.+
146 Nimekuitia wewe. Uniokoe!+
Nami nitavishika vikumbusho vyako.+
147 Nimeamka mapema wakati wa mapambazuko ya asubuhi,+ ili nipate kulilia msaada.+
Kwa maana nimeyangojea maneno yako.+
148 Macho yangu yametangulia makesha ya usiku,+
Ili nijishughulishe na neno lako.+
149 Uisikie sauti yangu kulingana na fadhili zako zenye upendo.+
Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na uamuzi wako wa hukumu.+
150 Wale wanaofuatilia mwenendo mpotovu+ wamekaribia;
Wameenda mbali na sheria yako.+
151 Wewe uko karibu, Ee Yehova+
Na amri zako zote
ni kweli.+
152 Zamani za kale nimejua baadhi ya vikumbusho vyako,+
Kwa maana umeviwekea msingi tangu zamani za kale.+
ר [Rehsh]
153 Uone mateso yangu na kuniokoa;+
Kwa maana sijaisahau sheria yako mwenyewe.+
154 Uendeshe kesi yangu na kunikomboa;+
Unihifadhi hai kulingana na neno lako.+
155 Wokovu uko mbali sana na waovu,+
Kwa maana hawajayatafuta masharti yako.+
156 Rehema zako ni nyingi, Ee Yehova.+
Unihifadhi hai kulingana na maamuzi yako ya hukumu.+
157 Wanaonitesa na adui zangu ni wengi.+
Sijaondoka katika vikumbusho vyako.+
158 Nimewaona wale wanaotenda kwa hila,+
Nami nimechukizwa, kwa sababu hawakulishika neno lako.+
159 Uone kwamba nimeyapenda maagizo yako.+
Ee Yehova, unihifadhi hai kulingana na fadhili zako zenye upendo.+
160 Kiini cha neno lako ni kweli,+
Na kila uamuzi wako wa hukumu wa uadilifu ni wa mpaka wakati usio na kipimo.+
ש [Sin] au [Shin]
161 Wakuu wamenitesa bila sababu,+
Lakini moyo wangu umekuwa ukiyahofu maneno yako.+
162 Ninafurahi kwa sababu ya neno lako+
Kama vile mtu anavyofanya anapopata nyara nyingi.+
163 Nimeuchukia uwongo,+ nami naendelea kuuchukia.+
Sheria yako nimeipenda.+
164 Mara saba wakati wa mchana nimekusifu+
Kwa sababu ya maamuzi yako ya hukumu ya uadilifu.+
165 Wale wanaoipenda sheria yako wana amani nyingi,+
Na hakuna kitu cha kuwakwaza.+
166 Nimeutumainia wokovu wako, Ee Yehova,+
Nami nimezitenda amri zako.+
167 Nafsi yangu imeshika vikumbusho vyako,+
Nami navipenda sana.+
168 Nimeyashika maagizo yako na vikumbusho vyako,+
Kwa maana njia zangu zote ziko mbele zako.+
ת [Taw]
169 Kilio changu cha kusihi na kije karibu mbele zako,
Ee Yehova.+
Kulingana na neno lako, nifanye nielewe.+
170 Ombi langu la kutaka kibali na liingie mbele zako.+
Kulingana na neno lako, unikomboe.+
171 Midomo yangu na ibubujike sifa,+
Kwa maana unanifundisha masharti yako.+
172 Ulimi wangu na uimbe maneno yako,+
Kwa maana amri zako zote ni uadilifu.+
173 Mkono wako na unisaidie,+
Kwa sababu nimeyachagua maagizo yako.+
174 Nimeutamani wokovu wako, Ee Yehova,+
Nami naipenda sheria yako.+
175 Nafsi yangu na iendelee kuishi na kukusifu,+
Nayo maamuzi yako ya hukumu na yanisaidie.+
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea.+ Umtafute mtumishi wako,+
Kwa maana sijazisahau amri zako.+