Zaburi Wimbo wa Mipando. 120 Nilimwita Yehova katika taabu yangu,+Naye akanijibu.+ 2 Ee Yehova, uikomboe nafsi yangu kutokana na midomo ya uwongo,+Kutokana na ulimi wenye ujanja.+ 3 Mtu atakupa nini, na mtu atakuongezea nini,Ewe ulimi wenye ujanja?+ 4 Mishale iliyonolewa ya mwanamume mwenye nguvu,+Pamoja na makaa yanayowaka moto ya miretemu.+ 5 Ole wangu, kwa maana nimekaa nikiwa mgeni katika Mesheki!+Nimekaa pamoja na mahema ya Kedari.+ 6 Kwa maana nafsi yangu imekaa kwa muda mrefu+Pamoja na watu wanaochukia amani.+ 7 Nasimama kwa ajili ya amani;+ lakini ninaposema,Wao wanataka vita.+