Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 6:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 Ndipo Yoashi+ akawaambia wote waliosimama kumpinga:+ “Je, ninyi ndio mtakaomtetea kisheria Baali ili kuona kama ninyi wenyewe mnaweza kumwokoa? Yeyote atakayemtetea kisheria anapaswa kuuawa asubuhi hii.+ Ikiwa yeye ni Mungu,+ acheni ajitetee mwenyewe kisheria,+ kwa sababu mtu fulani amebomoa madhabahu yake.”

  • 1 Samweli 24:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na Yehova atakuwa mwamuzi, naye atahukumu kati yangu na wewe, naye ataona na kufanya kesi+ kwa ajili yangu na kunihukumu ili kuniweka huru kutoka mkononi mwako.”

  • Zaburi 35:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Endesha kesi yangu dhidi ya wapinzani wangu, Ee Yehova;+

      Upigane na wale wanaopigana nami.+

  • Zaburi 43:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Unihukumu,+ Ee Mungu,

      Na uendeshe kesi+ yangu dhidi ya taifa lisilo shikamanifu.

      Uniokoe kutoka kwa mtu wa udanganyifu na mwenye kukosa uadilifu.+

  • Methali 22:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Kwa maana Yehova mwenyewe atatetea kesi yao,+ naye hakika atawanyang’anya nafsi wale wanaowanyang’anya.+

  • Methali 23:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kwa maana Mkombozi wao ana nguvu; yeye mwenyewe atatetea kesi yao dhidi yako wewe.+

  • Yeremia 50:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 Mkombozi wao ni mwenye nguvu,+ Yehova wa majeshi ndilo jina lake.+ Bila shaka ataendesha kesi yao,+ ili aipe nchi utulivu+ na kuwafadhaisha wakaaji wa Babiloni.”+

  • Maombolezo 3:59
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 59 Umeona kosa nililotendewa, Ee Yehova.+ Tafadhali fanya hukumu kwa ajili yangu.+

  • Mika 7:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Ghadhabu ya Yehova nitaivumilia​—​kwa maana nimemtendea dhambi+​—​mpaka atakapoendesha kesi yangu na kutekeleza haki kwa ajili yangu.+ Atanileta kwenye nuru; nitautazama uadilifu wake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki