Zaburi
Na uendeshe kesi+ yangu dhidi ya taifa lisilo shikamanifu.
Uniokoe kutoka kwa mtu wa udanganyifu na mwenye kukosa uadilifu.+
2 Kwa maana wewe ni Mungu wa ngome yangu.+
Kwa nini umenitupilia mbali?
Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?+
3 Tuma nuru yako na kweli yako.+
Na hivyo vyenyewe viniongoze.+
Navyo vinilete kwenye mlima wako mtakatifu na kwenye maskani yako kuu.+