Zaburi
Kwa kiongozi. Ya wana wa Kora.+ Maskili.
44 Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu,
Mababu zetu wenyewe wametusimulia+
Utendaji ambao ulifanya katika siku zao,+
Siku za zamani za kale.+
2 Wewe mwenyewe kwa mkono wako uliwafukuzia mbali mataifa,+
Nawe ukawapanda hao badala yao.+
Ukavunja vikundi vya mataifa na kuwafukuza.+
3 Kwa maana hawakuimiliki nchi hiyo kwa upanga wao wenyewe,+
Wala wokovu haukuletwa kwa mkono wao wenyewe.+
Kwa maana ulikuwa ni mkono wako wa kuume,+ naam, mkono wako na nuru ya uso wako,
Kwa sababu ulipendezwa nao.+
5 Kupitia wewe tutawasukuma wapinzani wetu;+
Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaosimama dhidi yetu.+
7 Kwa maana ulituokoa kutoka kwa wapinzani wetu,+
Nawe ukawafanya waone aibu wale wanaotuchukia vikali.+
10 Wewe unaendelea kutufanya tugeuke kutoka kwa adui zetu,+
Na wale wanaotuchukia vikali wamejinyakulia vitu.+
13 Unatuweka kuwa shutuma kwa jirani zetu,+
Kuwa dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka pande zote.+
14 Umetufanya kuwa neno la kimethali kati ya mataifa,+
Kuwa kitu cha kutikisiwa kichwa kati ya vikundi vya mataifa.+
16 Kwa sababu ya sauti ya mtu anayeshutumu na kusema vibaya,
Kwa sababu ya adui na mtu anayejilipizia kisasi.+
17 Yote hayo ndiyo yametujia, nasi hatujakusahau,+
Wala hatujatenda kwa njia ya uwongo katika agano lako.+
18 Moyo wetu haujageuka nyuma kwa kukosa imani,+
Wala hatua za miguu yetu hazitoki katika njia yako.+