Zaburi
KITABU CHA PILI
Kwa kiongozi. Maskili kwa ajili ya wana wa Kora.+
2 Kwa kweli nafsi yangu ina kiu kwa ajili ya Mungu,+ kwa ajili ya Mungu aliye hai.+
Ni wakati gani nitakapokuja nionekane mbele za Mungu?+
3 Machozi yangu yamekuwa chakula changu mchana na usiku,+
Huku wakiniambia mchana kutwa: “Mungu wako yuko wapi?”+
4 Nitakumbuka mambo haya, nami nitaimimina nafsi yangu iliyo ndani yangu.+
Kwa maana nilikuwa nikipita pamoja na watu wengi,
Nilikuwa nikitembea polepole mbele yao kwenda kwenye nyumba ya Mungu,+
Kwa sauti ya vigelegele vya shangwe na shukrani,+
Ya umati unaofanya sherehe.+
5 Kwa nini umekata tamaa, Ee nafsi yangu,+
Na kwa nini una msukosuko ndani yangu?+
Mngojee Mungu,+
Kwa maana bado nitamsifu kuwa ndiye wokovu wangu mkuu.+
6 Ee Mungu wangu, nafsi yangu mwenyewe imekata tamaa ndani yangu.+
Ndiyo sababu ninakukumbuka,+
Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,+
Kutoka katika ule mlima mdogo.+
7 Kilindi cha maji kinaita kilindi cha maji
Kwa sauti ya mabubujiko yako ya maji.
Mashuu yako yote na mawimbi yako+—
Yamepita juu yangu.+
8 Wakati wa mchana Yehova ataamuru fadhili zake zenye upendo,+
Na wakati wa usiku wimbo wake utakuwa nami;+
Kutakuwako sala kwa Mungu wa uhai wangu.+
9 Nitamwambia Mungu mwamba wangu:+
“Kwa nini umenisahau?+
Kwa nini natembea kwa huzuni kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?”+