Methali
23 Ukiketi kula pamoja na mfalme, fikiria sana kilicho mbele yako,+ 2 nawe ujitie kisu kooni ikiwa una nafsi yenye tamaa.+ 3 Usionyeshe kuwa unatamani vyakula vyake vitamu, kwa maana ni vyakula vya uwongo.+
4 Usijitaabishe kutafuta utajiri.+ Acha kutegemea uelewaji wako mwenyewe.+ 5 Je, umeukazia macho, nao si kitu?+ Kwa maana hakika huo hujifanyia mabawa kama yale ya tai na kuruka kuelekea mbinguni.+
6 Usile chakula cha mtu mwenye jicho lisilo na ukarimu,+ wala kujionyesha kuwa unatamani vyakula vyake vitamu.+ 7 Kwa maana yeye ni kama mtu ambaye amefikiria ndani ya nafsi yake.+ “Kula na kunywa,” anakuambia, lakini moyo wake haupo pamoja nawe.+ 8 Utatapika tonge ulilokula, nawe utakuwa umepoteza maneno yako matamu.+
9 Usiseme masikioni mwa mtu mjinga,+ kwa maana atayadharau maneno yako yenye busara.+
10 Usiusogeze nyuma mpaka wa zamani za kale,+ wala usiingie katika shamba la wavulana wasio na baba.+ 11 Kwa maana Mkombozi wao ana nguvu; yeye mwenyewe atatetea kesi yao dhidi yako wewe.+
12 Elekeza moyo wako kwenye nidhamu na sikio lako kwenye maneno ya ujuzi.+
13 Usimnyime mvulana nidhamu.+ Ukimpiga kwa fimbo, hatakufa. 14 Inakupasa wewe mwenyewe umpige kwa fimbo, upate kuikomboa nafsi yake na Kaburi.*+
15 Mwanangu, ikiwa moyo wako umekuwa na hekima,+ moyo wangu utashangilia, naam, moyo wangu.+ 16 Na figo zangu zitashangilia midomo yako inaposema mambo manyoofu.+
17 Moyo wako usiwaonee wivu watenda-dhambi,+ lakini umwogope Yehova mchana kutwa.+ 18 Kwa maana ndipo kutakapokuwa na wakati ujao,+ na tumaini lako mwenyewe halitakatiliwa mbali.+
19 Ewe mwanangu, sikia uwe na hekima, na kuuongoza moyo wako katika njia hiyo.+
20 Usiwe kati ya watu wanaokunywa divai mno,+ kati ya watu wanaokula nyama kwa ulafi.+ 21 Kwa maana mlevi na mlafi watakuwa maskini,+ na kusinzia kutamvika mtu nguo zilizopasuka.+
22 Msikilize baba yako aliyekuzaa,+ wala usimdharau mama yako kwa sababu tu amezeeka.+ 23 Nunua kweli+ wala usiiuze—hekima na nidhamu na uelewaji.+ 24 Baba ya mtu mwadilifu hakika atakuwa na shangwe;+ na mtu anayekuwa baba ya mwenye hekima atamshangilia pia.+ 25 Baba yako na mama yako watashangilia, naye mama aliyekuzaa atakuwa na shangwe.+
26 Mwanangu, nipe moyo wako, nayo macho yako na yapendezwe na njia zangu mwenyewe.+ 27 Kwa maana kahaba ni shimo refu+ na mwanamke mgeni ni kisima chembamba. 28 Kwa kweli, yeye huvizia, kama mnyang’anyi;+ naye huwaongeza wenye hila katika wanadamu.+
29 Ni nani aliye na ole? Ni nani aliye na wasiwasi? Ni nani aliye na ugomvi?+ Ni nani aliye na mahangaiko? Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? Ni nani aliye na macho mazito? 30 Ni wale wanaokaa muda mrefu kwenye divai,+ wale wanaoenda kutafuta divai iliyochanganyika.+ 31 Usiitazame divai inapotoa rangi nyekundu, inapochemka katika kikombe, inaposhuka taratibu. 32 Mwisho wake inauma kama nyoka,+ nayo hutoa sumu kama nyoka.+ 33 Macho yako mwenyewe yataona mambo mageni, nao moyo wako mwenyewe utasema mambo yaliyopotoka.+ 34 Nawe utakuwa kama mtu anayelala katikati ya bahari, kama mtu anayelala juu ya mlingoti.+ 35 “Wamenipiga, lakini sikuwa mgonjwa; wamenichapa, lakini sikujua; Nitaamka wakati gani?+ Bado nitaitafuta hata zaidi.”+