Methali
24 Usiwaonee wivu watu wabaya,+ wala usitamani kuingia pamoja nao.+ 2 Kwa maana moyo wao huendelea kutafakari juu ya uporaji, nayo midomo yao huendelea kuongea juu ya matata.+
3 Nyumba hujengwa kwa hekima,+ na kwa utambuzi itasimamishwa imara.+ 4 Na kwa ujuzi vyumba vya ndani vitajazwa vitu vyote vyenye thamani na vyenye kupendeza.+
5 Mtu mwenye hekima katika nguvu ni mwanamume,+ na mtu mwenye ujuzi anaimarisha nguvu.+ 6 Kwa maana kwa mwongozo stadi utaendeleza vita vyako,+ na kwa wingi wa washauri kuna wokovu.+
7 Kwa mpumbavu, hekima ya kweli iko juu mno;+ hatafungua kinywa chake langoni.
8 Yeyote anayepanga hila ya kufanya ubaya ataitwa fundi wa mawazo ya uovu.+
9 Mwenendo mpotovu wa upumbavu ni dhambi,+ na mwenye dhihaka ni chukizo kwa wanadamu.+
10 Je, umejionyesha kuwa umevunjika moyo siku ya taabu?+ Nguvu zako zitakuwa chache.
11 Wakomboe wale wanaopelekwa kwenye kifo; na uwazuie wale wanaopepesuka wakielekea kuchinjwa.+ 12 Ikiwa utasema: “Tazama! Hatukujua hili,”+ je, yule anayeipima mioyo hatatambua hilo,+ na yule anayeichunguza nafsi yako mwenyewe hatajua+ hilo naye hakika hatamlipa mtu wa udongo kulingana na utendaji wake?+
13 Mwanangu, kula asali, kwa maana ni njema; asali tamu ya sega na iwe katika kaakaa lako.+ 14 Vivyo hivyo, ijue hekima kwa ajili ya nafsi yako.+ Ikiwa umeipata, basi kuna wakati ujao, na tumaini lako mwenyewe halitakatiliwa mbali.+
15 Usijifiche ili kushambulia makao ya mwadilifu kama anavyofanya mwovu;+ usipore mahali pake pa kupumzikia.+ 16 Kwa maana huenda mwadilifu akaanguka hata mara saba, naye hakika atasimama;+ lakini waovu watakwazwa na msiba.+
17 Adui yako anapoanguka, usishangilie; naye anapokwazwa, moyo wako usiwe na shangwe,+ 18 ili Yehova asipate kuona jambo hilo nalo liwe baya machoni pake, naye aigeuzie hasira yake mbali naye.+
19 Usiwake kwa hasira juu ya watenda-maovu. Usiwaonee wivu watu waovu.+ 20 Kwa maana mtu yeyote mbaya hatakuwa na wakati ujao;+ taa ya watu waovu itazimwa.+
21 Mwanangu, mwogope Yehova na mfalme.+ Usishirikiane na watu wanaotaka badiliko.+ 22 Kwa maana msiba wao utakuja ghafula,+ hivi kwamba ni nani anayejua juu ya kuangamizwa kwa watu wanaotaka badiliko?+
23 Maneno haya pia ni kwa ajili ya watu wenye hekima:+ Kuonyesha upendeleo katika hukumu si jambo zuri.+
24 Anayemwambia mtu mwovu: “Wewe ni mwadilifu,”+ watu watamlaani, na vikundi vya mataifa vitamshutumu. 25 Lakini kwao wanaomkaripia mambo yatakuwa yenye kupendeza,+ nayo baraka ya mema itawajia.+ 26 Anayejibu kwa njia ya unyoofu atabusu midomo.+
27 Tayarisha kazi yako huko nje, uifanye tayari kwa ajili yako shambani.+ Kisha ujenge nyumba yako.
28 Usimshuhudie mwenzako pasipo msingi.+ Ndipo ungekuwa mpumbavu kwa midomo yako.+ 29 Usiseme: “Nitamtendea kama vile tu alivyonitendea.+ Nitamlipa kila mtu kulingana na tendo lake.”+
30 Nilipitia kando ya shamba la mtu mvivu+ na kando ya shamba la mizabibu la mtu aliyepungukiwa moyoni.+ 31 Na tazama! Lote lilizaa magugu.+ Uso wake ulifunikwa na miiba, nao ukuta wake wa mawe ulikuwa umebomolewa.+
32 Basi nikaona, mimi mwenyewe; nikaanza kutia jambo hilo moyoni;+ nikaona, nikaikubali nidhamu:+ 33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo, kukunja mikono kidogo ili kulala,+ 34 nao umaskini wako utakuja kama mnyang’anyi wa njia kuu na uhitaji wako kama mwanamume mwenye silaha.+