Methali
25 Hizi pia ni methali za Sulemani+ ambazo watu wa Hezekia, mfalme wa Yuda,+ walinakili:
2 Utukufu wa Mungu ni kuweka jambo kuwa siri,+ nao utukufu wa wafalme ni kuchunguza jambo kabisa.+
3 Mbingu kwa kimo na dunia kwa kina,+ na moyo wa wafalme,+ hayo hayachunguziki.+
4 Takataka na iondolewe kwenye fedha, na yote itatoka ikiwa safi.+
5 Mwovu na aondolewe mbele ya mfalme,+ na kiti chake cha ufalme kitafanywa imara kwa uadilifu wenyewe.+
6 Usijiheshimu mwenyewe mbele ya mfalme,+ wala usisimame mahali pa wakuu.+ 7 Kwa maana ni afadhali yeye akuambie: “Njoo hapa,”+ kuliko akushushe mbele ya mtu mwenye cheo ambaye macho yako yamemwona.+
8 Usiende kwa haraka kufanya kesi, ili sasa swali lisiwe utafanya nini mwishowe mwenzako anapokuaibisha.+ 9 Jitetee kwa mwenzako,+ wala usifunue mazungumzo ya siri ya mwingine;+ 10 ili anayesikiliza asikuaibishe na habari yako mbaya iwe haiwezi kufutwa.
11 Neno linalosemwa wakati unaofaa ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu kwenye chombo cha fedha kilichopambwa.+
12 Pete ya dhahabu na pambo la dhahabu ya pekee, ndivyo alivyo mkaripiaji mwenye hekima kwenye sikio linalosikia.+
13 Kama baridi ya theluji+ siku ya mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wanaomtuma, kwa maana yeye huiburudisha nafsi ya mabwana wake.+
14 Kama wingu la mvuke na upepo bila mvua ndivyo alivyo mtu anayejisifu kwa uwongo juu ya zawadi.+
15 Kwa subira kiongozi hushawishiwa, na ulimi wa upole unaweza kuvunja mfupa.+
16 Je, umepata asali?+ Kula kiasi cha kukutosha, ili usiile kupita kiasi kisha uitapike.+
17 Fanya mguu wako uwe haba nyumbani kwa mwenzako, asije akakuchoka na hakika akuchukie.
18 Kama rungu ya vita na upanga na mshale mkali ndivyo alivyo mtu anayemshuhudia mwenzake kwa uwongo.+
19 Uhakika katika mtu mwenye hila siku ya taabu, ni kama jino lililovunjika na mguu ulioteguka.+
20 Yeye anayevua nguo siku ya baridi ni kama siki kwenye magadi na kama mwimbaji anayemwimbia mtu aliye na moyo wenye huzuni.+
21 Ikiwa mtu anayekuchukia ana njaa, mpe mkate ale; na ikiwa ana kiu, mpe maji anywe.+ 22 Kwa maana unakusanya makaa ya moto juu ya kichwa chake,+ na Yehova mwenyewe atakupa thawabu.+
23 Upepo wa kaskazini hutokeza mvua+ kana kwamba kwa uchungu wa kuzaa; nao ulimi unaofunua siri hutokeza uso ulioshutumiwa.+
24 Ni afadhali kukaa pembeni mwa paa kuliko kukaa pamoja na mke mgomvi, ingawa ni katika nyumba moja.+
25 Kama maji baridi kwa nafsi iliyochoka+ ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.+
26 Mwadilifu anapopepesuka mbele ya mwovu ni kama bubujiko la maji yaliyochafuka na kisima kilichoharibika.+
27 Si vizuri kula asali nyingi mno;+ na watu kujitafutia utukufu wao wenyewe, je, huo ni utukufu?+
28 Mtu asiyezuia roho yake ni kama jiji lililobomolewa, lisilo na ukuta.+