Methali
26 Kama theluji wakati wa kiangazi na kama mvua wakati wa mavuno,+ kadhalika mtu mjinga hastahili utukufu.+
2 Kama ndege alivyo na sababu ya kukimbia na mbayuwayu alivyo na sababu ya kuruka, hivyo laana haiji bila sababu halisi.+
3 Mjeledi ni wa farasi,+ lijamu+ ni ya punda, nayo fimbo ni ya mgongo wa watu wajinga.+
4 Usimjibu mtu yeyote mjinga kulingana na upumbavu wake, ili wewe nawe usiwe sawa na yeye.+
5 Mjibu mjinga kulingana na upumbavu wake, ili asipate kuwa mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe.+
6 Kama mtu anayekata-kata miguu yake, kama mtu anayekunywa jeuri tupu, ndivyo alivyo mtu anayetia mambo mikononi mwa mjinga.+
7 Je, miguu ya kilema imeteka maji? Ikiwa ndivyo basi kinywani mwa watu wajinga mna methali.+
8 Kama mtu anayefungia jiwe kwenye rundo la mawe, ndivyo alivyo mtu anayempa mtu mjinga utukufu.+
9 Kama gugu lenye miiba lilivyoingia katika mkono wa mlevi, ndivyo na methali ndani ya kinywa cha watu wajinga.+
10 Kama mpiga-mishale anayechoma kila kitu ndivyo alivyo mtu anayeajiri mjinga+ au anayeajiri wapita-njia.
11 Kama mbwa anayerudia matapiko yake, ndivyo mtu mjinga anavyorudia upumbavu wake.+
12 Je, umemwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe?+ Kuna tumaini zaidi kwa mjinga+ kuliko kwake.
13 Mvivu amesema: “Kuna mwana-simba njiani, simba katikati ya viwanja vya watu wote.”+
14 Kama vile mlango unavyogeuka katika bawaba zake, ndivyo alivyo mvivu katika kitanda chake.+
15 Mvivu ameutia mkono wake katika bakuli la karamu; amechoka mno asiweze kuurudisha kwenye kinywa chake.+
16 Machoni pake mwenyewe mvivu ni mwenye hekima+ kuliko watu saba wanaojibu kwa kutumia akili.
17 Mpita-njia yeyote anayekasirishwa na ugomvi usio wake ni kama mtu anayemshika mbwa masikio.+
18 Kama mtu mwenye wazimu anayetupa silaha za moto,+ mishale na kifo, 19 ndivyo alivyo mtu ambaye amemdanganya mwenzake na kusema: “Je, sikuwa nikifanya mzaha tu?”+
20 Pasipo na kuni moto huzimika, na pasipo na mchongezi ugomvi hutulia.+
21 Kama kuongeza makaa kwenye makaa yanayowaka na kuni kwenye moto, ndivyo mtu mgomvi hufanya ugomvi+ uwake moto.
22 Maneno ya mchongezi ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa, vinavyoingia katika sehemu za ndani kabisa za tumbo.+
23 Kama fedha inayofunika kipande cha chombo cha udongo, ndivyo ilivyo midomo yenye bidii pamoja na moyo mbaya.+
24 Kwa midomo yake, mtu mwenye chuki hujificha asitambuliwe, lakini ndani yake huweka udanganyifu.+ 25 Ijapokuwa yeye huifanya sauti yake kuwa yenye kupendeza,+ usimwamini,+ kwa maana mna machukizo saba+ moyoni mwake. 26 Chuki hufunikwa kwa udanganyifu. Ubaya wake utafunuliwa katika kutaniko.+
27 Anayechimba shimo ataanguka ndani yake,+ naye anayeviringisha jiwe—litarudi kwake.+
28 Ulimi wa uwongo humchukia mtu aliyepondwa nao,+ na kinywa chenye kubembeleza husababisha mapinduzi.+