Methali
22 Ni afadhali kuchagua jina badala ya utajiri mwingi;+ kibali ni bora kuliko hata fedha na dhahabu.+
2 Mtu tajiri na maskini wamekutana.+ Mtengenezaji wao wote ni Yehova.+
3 Mtu mwerevu ni yule ambaye ameona msiba na kujificha,+ lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.+
4 Matokeo ya unyenyekevu na kumwogopa Yehova ni utajiri na utukufu na uzima.+
5 Miiba na mitego imo katika njia ya mpotovu;+ yeye anayeilinda nafsi yake hukaa mbali nayo.+
6 Mlee mvulana kulingana na njia inayomfaa;+ hata atakapozeeka hatageuka kando na kuiacha.+
7 Mtu tajiri ndiye huwatawala maskini,+ na mkopaji ni mtumishi wa mtu anayemkopesha.+
8 Yeye anayepanda ukosefu wa uadilifu atavuna madhara,+ lakini fimbo ya ghadhabu yake itafikia mwisho wake.+
9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, kwa maana amempa mtu wa hali ya chini chakula chake.+
10 Mfukuze mwenye dhihaka, ili ugomvi utoke na ili mashtaka ya kisheria na ukosefu wa heshima vikome.+
11 Anayependa usafi wa moyo+—mfalme atakuwa mwenzake kwa sababu ya uvutio wa midomo yake.+
12 Macho ya Yehova mwenyewe yamelinda ujuzi,+ lakini yeye hupindua maneno ya mwenye hila.+
13 Mvivu amesema:+ “Kuna simba nje!+ Nitauawa katikati ya viwanja vya watu wote!”
14 Kinywa cha wanawake wageni ni shimo refu.+ Anayeshutumiwa na Yehova ataanguka ndani yake.+
15 Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa mvulana;+ fimbo ya nidhamu ndiyo itakayouondolea mbali.+
16 Anayempunja mtu wa hali ya chini ili ajipatie vitu vingi,+ pia yeye anayempa tajiri, hakika atakuwa na uhitaji.+
17 Tega sikio lako usikie maneno ya wenye hekima,+ ili kuutia moyo wako katika ujuzi wangu.+ 18 Kwa maana inapendeza kwamba uyaweke tumboni mwako,+ ili yapate kufanywa imara midomoni mwako.+
19 Ili uhakika wako uuweke kwa Yehova,+ nimekupa wewe, naam, wewe, ujuzi leo.
20 Je, kufikia sasa sikukuandikia mashauri na ujuzi,+ 21 nikuonyeshe ukweli wa maneno ya kweli, ili urudishe maneno yaliyo kweli—kwa yule anayekutuma?+
22 Usimnyang’anye mtu wa hali ya chini kwa sababu yeye ni wa hali ya chini,+ wala usimkandamize mwenye kuteseka langoni.+ 23 Kwa maana Yehova mwenyewe atatetea kesi yao,+ naye hakika atawanyang’anya nafsi wale wanaowanyang’anya.+
24 Usishirikiane na mtu yeyote mwenye mazoea ya kukasirika;+ wala usiende pamoja na mtu wa mifoko ya ghadhabu, 25 ili usizoee njia yake na hakika uiwekee nafsi yako mtego.+
26 Usiwe kati ya wale wanaopeana mikono+ kwa mapatano, kati ya wale wanaoweka dhamana kwa ajili ya mikopo.+ 27 Ikiwa huna kitu cha kulipa, kwa nini achukue kitanda chako kutoka chini yako?
28 Usiusogeze nyuma mpaka wa zamani za kale, uliowekwa na mababu zako.+
29 Je, umemwona mtu stadi katika kazi yake? Yeye atasimama mbele ya wafalme;+ hatasimama mbele ya watu wa kawaida.