1 Samweli
24 Na ikawa kwamba mara tu Sauli aliporudi baada ya kuwafuatilia Wafilisti,+ wakamletea habari, wakisema: “Tazama! Daudi yuko katika nyika ya En-gedi.”+
2 Na Sauli akachukua watu elfu tatu waliochaguliwa+ kutoka katika Israeli yote kwenda kumtafuta Daudi+ na watu wake juu ya miamba iliyo wazi ya mbuzi wa milimani.+ 3 Mwishowe akafika kwenye mazizi ya mawe ya kondoo kando ya barabara, mahali ambapo palikuwa na pango. Basi Sauli akaingia ndani kwenda haja,+ huku Daudi na watu wake wakiwa katika sehemu za nyuma kabisa za pango hilo,+ wakiwa wameketi. 4 Na watu wa Daudi wakaanza kumwambia: “Hii ndiyo siku ambayo Yehova anakuambia, ‘Tazama! Ninamtia adui yako mkononi mwako,+ nawe umtendee kama inavyoonekana vema machoni pako.’”+ Kwa hiyo Daudi akasimama, akakata kimyakimya upindo wa koti lisilo na mikono la Sauli. 5 Lakini baadaye moyo wa Daudi ukaendelea kumchoma+ kwa sababu alikuwa amekata upindo wa lile koti la Sauli. 6 Basi akawaambia watu wake: “Ni jambo lisilowaziwa kwangu, kwa maoni ya Yehova, kwamba nimfanyie bwana wangu jambo hili, mtiwa-mafuta+ wa Yehova, kwa kunyoosha mkono wangu juu yake, kwa kuwa yeye ni mtiwa-mafuta wa Yehova.”+ 7 Kwa hiyo Daudi akawatawanya watu wake kwa maneno hayo, naye hakuwaruhusu wamshambulie Sauli.+ Naye Sauli akainuka kutoka katika lile pango na kwenda zake.
8 Basi Daudi akainuka baadaye, akatoka nje ya lile pango na kumwita Sauli, akisema: “Bwana wangu+ mfalme!” Ndipo Sauli akatazama nyuma, naye Daudi akainama kifudifudi,+ akasujudu. 9 Na Daudi akaendelea kumwambia Sauli: “Kwa nini unayasikiliza maneno ya watu,+ wakisema, ‘Tazama! Daudi anatafuta kukudhuru’? 10 Tazama, leo macho yako yameona jinsi Yehova alivyokutia leo mkononi mwangu ndani ya pango; na mtu fulani alisema nikuue,+ lakini nikakusikitikia, nikasema, ‘Sitanyoosha mkono wangu juu ya bwana wangu, kwa maana yeye ni mtiwa-mafuta+ wa Yehova.’ 11 Basi ona baba yangu,+ ndiyo, ona mkononi mwangu upindo wa koti lako lisilo na mikono, kwa sababu nilipokata upindo wa koti lako, sikukuua. Ujue na kuona kwamba hakuna ubaya+ wowote wala maasi mkononi mwangu, nami sikutenda dhambi juu yako, huku wewe ukiivizia nafsi yangu ili kuiondolea mbali.+ 12 Yehova na ahukumu kati yangu na wewe;+ na Yehova anilipizie kisasi+ kutoka kwako, lakini mkono wangu mwenyewe hautakuja juu yako.+ 13 Kama vile inavyosema methali ya watu wa kale, ‘Katika waovu uovu utatoka,’+ lakini mkono wangu mwenyewe hautakuja juu yako. 14 Je, mfalme wa Israeli ametoka nje kumfuata nani? Unamfuatilia nani? Mbwa aliyekufa?+ Kiroboto mmoja?+ 15 Na Yehova atakuwa mwamuzi, naye atahukumu kati yangu na wewe, naye ataona na kufanya kesi+ kwa ajili yangu na kunihukumu ili kuniweka huru kutoka mkononi mwako.”
16 Na ikawa kwamba, mara tu Daudi alipomaliza kumwambia Sauli maneno hayo, Sauli akasema: “Je, hii ni sauti yako, Daudi mwanangu?”+ Naye Sauli akapaaza sauti yake, akalia.+ 17 Naye akamwambia Daudi: “Wewe ni mwadilifu kuliko mimi,+ kwa maana wewe ndiye umenitendea mema,+ nami ndiye nimekutendea uovu. 18 Nawe umefunua leo mema ambayo umenitendea kwa maana Yehova alinitia mkononi mwako,+ nawe hukuniua. 19 Kwa maana, mtu akimpata adui yake, je, atamwacha ashike njia aende zake salama?+ Basi Yehova mwenyewe atakupa thawabu ya mema,+ kwa kuwa leo umenitendea hivyo. 20 Na sasa tazama! Najua vema bila shaka kwamba wewe utatawala ukiwa mfalme,+ na kwamba ufalme wa Israeli utadumu mkononi mwako. 21 Basi sasa niapie kwa Yehova+ kwamba hutaukatilia mbali uzao wangu baada yangu na kwamba hutaliangamiza jina langu kutoka katika nyumba ya baba yangu.”+ 22 Kwa hiyo Daudi akamwapia Sauli, kisha Sauli akaenda nyumbani kwake.+ Naye Daudi na watu wake wakapanda, wakaenda mahali palipo pagumu kufikiwa.+