Maombolezo
א [ʼAʹleph]
3 Mimi ndiye mwanamume ambaye ameona mateso+ kwa sababu ya fimbo ya ghadhabu yake.
2 Mimi ndiye ameongoza, naye hunitembeza katika giza wala si katika nuru.+
3 Kwa kweli, yeye hugeuza tena na tena mkono wake juu yangu mchana kutwa.+
ב [Behth]
4 Amefanya nyama yangu na ngozi yangu ichakae.+ Amevunja mifupa yangu.+
5 Amejenga juu yangu, ili anizunguke+ kwa mmea wenye sumu+ pamoja na magumu.
6 Amenifanya niketi mahali penye giza+ kama watu waliokufa zamani.+
ג [Giʹmel]
7 Amenizuia kana kwamba kwa ukuta wa mawe, ili nisiweze kutoka.+ Amefanya pingu zangu za shaba+ ziwe nzito.
8 Pia, nikiomba na kulilia msaada, yeye kwa kweli huizuia sala yangu.+
9 Amezuia njia zangu kwa mawe yaliyochongwa.+ Amepotosha barabara zangu.+
ד [Daʹleth]
10 Kwangu, yeye ni kama dubu anayevizia,+ kama simba mafichoni.+
11 Amevuruga njia zangu, naye huniachilia niwe bure tu. Amenifanya niwe mtu aliyeachwa ukiwa.+
12 Amekanyaga upinde wake,+ naye huniweka niwe shabaha ya mshale.+
ה [Heʼ]
13 Ameingiza ndani ya figo zangu mishale, wana wa podo lake.+
14 Nimekuwa kitu cha kuchekwa+ na watu wote wanaonipinga, nimekuwa kichwa cha wimbo wao mchana kutwa.+
15 Amenishibisha vitu vichungu.+ Amenijaza pakanga.+
ו [Waw]
16 Naye huvunja meno yangu kwa changarawe.+ Amenifanya nijikunje katika majivu.+
17 Wewe pia hunitupilia mbali ili nafsi yangu isiwe na amani. Nimepoteza kumbukumbu ya mema.+
18 Nami huendelea kusema: “Utukufu wangu umeangamia, na tarajio langu kutoka kwa Yehova.”+
ז [Zaʹyin]
19 Ukumbuke mateso yangu na hali yangu ya kukosa makao,+ pakanga na mmea wenye sumu.+
20 Hakika nafsi yako itakumbuka na kuinama juu yangu.+
21 Hili ndilo nitakalokumbuka moyoni mwangu.+ Ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kungojea.+
ח [Chehth]
22 Ni kutokana na matendo ya fadhili zenye upendo+ za Yehova kwamba hatujaisha,+ kwa maana hakika rehema zake hazitakoma.+
23 Ni mapya kila asubuhi.+ Uaminifu wako ni mwingi.+
24 “Yehova ni fungu langu,”+ nafsi yangu imesema, “ndiyo sababu nitaonyesha mtazamo wa kumngojea.”+
ט [Tehth]
25 Yehova ni mwema kwa yule anayemtumaini,+ kwa nafsi inayoendelea kumtafuta.+
26 Ni jambo jema kwa mtu kuungojea,+ ndiyo, kimyakimya,+ wokovu wa Yehova.+
27 Ni jambo jema kwa mwanamume kuchukua nira wakati wa ujana wake.+
י [Yohdh]
28 Acha aketi katika upweke na kukaa kimya,+ kwa sababu ameweka kitu fulani juu yake.+
29 Acha atie kinywa chake mavumbini.+ Labda kuna tumaini fulani.+
30 Acha ampe shavu lake yule anayempiga.+ Acha apate shibe yake ya shutuma.+
כ [Kaph]
31 Kwa maana Yehova hataendelea kuwatupilia mbali watu mpaka wakati usio na kipimo.+
32 Kwa maana, ijapokuwa ameleta huzuni,+ hakika pia ataonyesha rehema kulingana na wingi wa fadhili zake zenye upendo.+
33 Kwa maana si kutoka moyoni mwake mwenyewe kwamba amewatesa au kuwahuzunisha wana wa binadamu.+
ל [Laʹmedh]
34 Kuponda wafungwa wote wa dunia+ chini ya miguu ya mtu,+
35 Kugeuza kando hukumu ya mwanamume mbele za uso wa Aliye Juu Zaidi,+
36 Kupotosha mtu katika kesi yake, Yehova mwenyewe hayakubali mambo hayo.+
מ [Mem]
37 Basi, ni nani amesema kwamba jambo litokee wakati Yehova mwenyewe hakuamuru?+
38 Mambo mabaya na yaliyo mema hayatoki katika kinywa cha Aliye Juu Zaidi.+
39 Mwanadamu aliye hai, mwanamume, anawezaje kuzoea kulalamika+ kwa sababu ya dhambi yake?+
נ [Nun]
40 Na tutafute njia zetu na kuzichunguza,+ nasi turudi kabisa kwa Yehova.+
41 Acheni tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu aliye mbinguni:+
42 “Sisi wenyewe tumekosa, nasi tumejiendesha kwa uasi.+ Wewe mwenyewe hukusamehe.+
ס [Saʹmekh]
43 Umeweka kizuizi kwa hasira usiweze kufikiwa,+ nawe unaendelea kutufuatilia.+ Umeua; hukuonyesha huruma yoyote.+
44 Umeweka kizuizi cha wingu kubwa usiweze kufikiwa,+ ili sala isiweze kupenya.+
45 Unatufanya tuwe takataka na uchafu katikati ya vikundi vya watu.”+
פ [Peʼ]
46 Adui zetu wote wamefungua vinywa vyao juu yetu.+
47 Hofu na shimo vimekuwa vyetu,+ ukiwa na kuvunjika.+
48 Jicho langu huendelea kutiririka vijito vya maji kwa sababu ya kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+
ע [ʽAʹyin]
49 Jicho langu limemwagika nalo halitatulia, hivi kwamba hakuna mapumziko,+
50 Mpaka Yehova atakapotazama chini na kuona kutoka mbinguni.+
51 Jicho langu limeitendea nafsi yangu vikali,+ kwa sababu ya binti wote wa jiji langu.+
צ [Tsa·dhehʹ]
52 Hakika adui zangu wameniwinda kama ndege,+ bila sababu.+
53 Wamenyamazisha uhai wangu shimoni kwenyewe,+ nao wakaendelea kunitupia mawe.
54 Maji yametiririka juu ya kichwa changu.+ Nimesema: “Hakika nitakatiliwa mbali!”+
ק [Qohph]
55 Nimeita jina lako, Ee Yehova, kutoka katika shimo la chini kabisa.+
56 Uisikilize sauti yangu.+ Usifiche sikio lako kwa ombi langu la kitulizo, kwa kilio changu cha kuomba msaada.+
57 Umekaribia katika siku ile ambayo niliendelea kukuita.+ Ukasema: “Usiogope.”+
ר [Rehsh]
58 Umechukua mashindano ya nafsi yangu, Ee Yehova.+ Umekomboa uhai wangu.+
59 Umeona kosa nililotendewa, Ee Yehova.+ Tafadhali fanya hukumu kwa ajili yangu.+
60 Umeona kisasi chao chote, fikira zao zote juu yangu.+
ש [Sin] au [Shin]
61 Umesikia shutuma zao, fikira zao zote juu yangu, Ee Yehova,+
62 Midomo ya wale wanaosimama kunipinga+ na kunong’ona kwao juu yangu mchana kutwa.+
63 Tazama wanapoketi na wanaposimama.+ Mimi ndiye kiini cha wimbo wao.+
ת [Taw]
64 Utawalipa tendo fulani, kulingana na kazi ya mikono yao, Ee Yehova.+
65 Utawapa dharau la moyo,+ laana yako kwao.+
66 Utawafuatilia katika hasira na kuwaangamiza+ chini ya mbingu za Yehova.+