29 Nawe kwa kweli utakuwa mtu anayepapasa-papasa katikati ya mchana, kama vile kipofu anavyopapasa-papasa gizani,+ nawe hutafanya njia zako zifanikiwe; nawe utakuwa mtu tu ambaye sikuzote hupunjwa na kunyang’anywa, pasipo mtu wa kukuokoa.+
9 Ndiyo sababu haki imekuwa mbali sana nasi, na uadilifu hautufikii. Tunaendelea kutumainia nuru, lakini, tazama! giza; kutumainia mwangaza, lakini tukazidi kutembea katika weusi unaoendelea.+
16 Mpeni Yehova Mungu wenu utukufu,+ kabla hajaleta giza+ na kabla miguu yenu haijagongana juu ya milima wakati wa jioni.+ Nanyi hakika mtaitumaini nuru,+ naye kwa kweli ataifanya iwe kivuli kizito;+ ataigeuza iwe giza zito.+