Maombolezo
א [ʼAʹleph]
2 Lo! jinsi Yehova katika hasira yake anavyomfunika kwa wingu binti Sayuni!+
Ameutupa chini uzuri wa Israeli+ kutoka mbinguni mpaka duniani.+
Naye hakumbuki kiti cha miguu+ yake katika siku ya hasira yake.
ב [Behth]
2 Yehova amemeza, hakuonyesha huruma juu ya makao+ yoyote ya Yakobo.
Katika hasira yake amebomoa ngome+ za binti Yuda.
ג [Giʹmel]
3 Katika joto kali la hasira amekata kila pembe ya Israeli.+
Amerudisha mkono wake wa kuume kutoka mbele ya adui;+
Naye huendelea kuwaka katika Yakobo kama moto unaowaka ambao umeteketeza kuzunguka pande zote.+
ד [Daʹleth]
4 Amekanyaga upinde wake kama adui.+ Mkono wake wa kuume+ umesimama mahali pake
Kama mpinzani,+ naye alizidi kuua wote wanaotamanika machoni.+
Kama moto, amemwaga ghadhabu+ yake katika hema+ la binti Sayuni.
ה [Heʼ]
5 Yehova amekuwa kama adui.+ Amemeza Israeli.+
Amemeza minara yake yote ya makao;+ ameziharibu ngome zake.+
Naye hujaza vilio na maombolezo katika binti Yuda.+
ו [Waw]
6 Naye hukitendea jeuri kibanda+ chake kama kile kilicho katika bustani.+ Ameiharibu sherehe yake.
Yehova amefanya sherehe+ na sabato kusahauliwa katika Sayuni,
Naye katika shutuma zake za hasira haheshimu mfalme wala kuhani.+
ז [Zaʹyin]
7 Yehova ameitupilia mbali madhabahu yake.+ Patakatifu pake amepakataa kwa dharau.+
Ametia katika mkono wa adui kuta za minara ya makao yake.+
Wamepaaza sauti zao ndani ya nyumba ya Yehova, kama katika siku ya sherehe.+
ח [Chehth]
8 Yehova amekusudia kuuharibu ukuta+ wa binti Sayuni.
Amenyoosha kamba ya kupimia.+ Hakurudisha mkono wake usimeze.+
Naye hufanya boma na ukuta kuomboleza.+ Zimedhoofika zote pamoja.
ט [Tehth]
9 Malango+ yake yamezama chini kabisa. Ameharibu na kuvunja mapingo yake vipande-vipande.
Mfalme wake na wakuu wake wako kati ya mataifa.+ Hakuna sheria.+
Manabii wake pia hawakupata maono kutoka kwa Yehova.+
י [Yohdh]
10 Wanaume wazee wa binti Sayuni wanaketi chini, ambapo wamenyamaza.+
Wametia mavumbi juu ya vichwa vyao.+ Wamejifunga nguo za magunia.+
Mabikira wa Yerusalemu wameinamisha vichwa vyao chini kabisa.+
כ [Kaph]
11 Macho yangu yamechoka kabisa kwa machozi matupu.+ Matumbo yangu yako katika msukosuko.+
Ini langu limemwagwa chini kabisa,+ kwa sababu ya anguko la binti ya watu wangu,+
Kwa sababu ya kuzimia kwa mtoto mchanga na yule anayenyonya katika viwanja vya watu wote vya jiji.+
ל [Laʹmedh]
12 Waliendelea kuwaambia mama zao: “Iko wapi nafaka na divai?”+
Kwa sababu ya kuzimia kwao kama mtu aliyeuawa katika viwanja vya watu wote vya jiji,
Kwa sababu ya nafsi yao kumwagwa kwenye vifua vya mama zao.
מ [Mem]
13 Nitakutumia kama shahidi juu ya nini? Nitakufananisha na nini, Ee binti Yerusalemu?+
Nitakulinganisha na nini, ili nikufariji, Ee binti Sayuni uliye bikira?+
Kwa maana mvunjiko+ wako ni mkubwa kama bahari. Ni nani anayeweza kukuponya?+
נ [Nun]
14 Manabii wako mwenyewe wameona kwa ajili yako maono ya ubatili na vitu visivyotosheleza,+
Nao hawakufunua kosa lako ili kuirudisha hali yako ya mateka,+
Bali waliendelea kuona kwa ajili yako maono ya matangazo yasiyo na faida na yanayopotosha.+
ס [Saʹmekh]
15 Wote wanaopita barabarani wamekupigia makofi.+
Wamepiga mluzi+ wa mshangao na kuendelea kutikisa vichwa+ vyao kwa sababu ya binti Yerusalemu, wakisema:
“Je, hili ndilo lile jiji ambalo walikuwa wakisema hivi kwa habari zake, ‘Hili ndilo ukamilifu wa uzuri, furaha ya dunia yote’?”+
פ [Peʼ]
16 Adui zako wote wamefungua vinywa vyao juu yako.+
Wamepiga mluzi wa mshangao na kuendelea kusaga meno.+ Wamesema: “Tutammeza.+
Kweli hii ndiyo siku ambayo tumeitumaini.+ Tumepata! Tumeona!”+
ע [ʽAʹyin]
17 Yehova amefanya alilokuwa nalo akilini mwake.+ Ametimiza neno lake,+
Aliloamuru tangu siku za kale.+ Amebomoa wala hakuonyesha huruma.+
Naye hufanya adui ashangilie juu yako.+ Ameinua juu pembe ya adui zako.+
צ [Tsa·dhehʹ]
18 Moyo wao umemlilia Yehova,+ Ee ukuta wa binti Sayuni.+
Yatiririshe machozi kama mto mchana na usiku.+
Usife ganzi. Mboni ya jicho lako isikae kimya.
ק [Qohph]
19 Simama! Lia wakati wa usiku mwanzoni mwa makesha ya kuamkia asubuhi.+
Mwaga moyo+ wako mbele za uso+ wa Yehova kama maji.
Mwinulie mikono+ yako kwa sababu ya nafsi ya watoto wako,
Wanaozimia kwa sababu ya njaa kwenye sehemu ya mbele ya barabara zote.+
ר [Rehsh]
20 Tazama, Ee Yehova, nawe umwone+ yule ambaye umemtendea vikali namna hii.
Je, wanawake waendelee kula uzao wao wenyewe, watoto waliozaliwa wakiwa wamekomaa,+
Au, je, kuhani na nabii wauawe ndani ya patakatifu pa Yehova?+
ש [Shin]
21 Mvulana na mwanamume mzee+ wamelala chini katika mavumbi ya barabara.+
Mabikira wangu na vijana wangu wenyewe wameanguka kwa upanga.+
Umeua katika siku ya hasira yako.+ Umechinja;+ hukuwa na huruma.+
ת [Taw]