30 Utakapokuwa katika dhiki kali na maneno yote haya yawe yamekupata mwishoni mwa siku hizo, basi utarudi kwa Yehova Mungu+ wako na kuisikiliza sauti yake.+
7 Mtu mwovu aiache njia yake,+ na mtu mwenye madhara ayaache mawazo yake;+ naye arudi kwa Yehova, ambaye atamwonyesha rehema,+ na kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.+
13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu;+ rudini kwa Yehova Mungu wenu, kwa maana yeye ana neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ naye hakika atajuta kwa sababu ya msiba huo.+