-
Nehemia 9:17Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Kwa hiyo wakakataa kusikiliza,+ wala hawakuyakumbuka+ matendo yako ya ajabu ambayo ulikuwa umewafanyia, bali wakafanya shingo zao kuwa ngumu+ na kujichagulia mkuu+ ili kurudi kwenye hali yao ya utumwa katika Misri. Lakini wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe,+ mwenye neema+ na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi+ wa fadhili zenye upendo, nawe hukuwaacha.+
-
-
Yona 4:2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Kwa hiyo akasali kwa Yehova na kusema: “Ah, sasa, Ee Yehova, je, hili halikuwa hangaiko langu, nilipokuwa katika nchi yangu mwenyewe? Ndiyo sababu nilikimbia na kwenda Tarshishi;+ kwa maana nilijua kwamba wewe ni Mungu mwenye neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ na mwenye kuujuta msiba.+
-