Zaburi
Sala ya Daudi
2 Uilinde nafsi yangu, kwa maana mimi ni mshikamanifu.+
Umwokoe mtumishi wako—wewe ni Mungu wangu—anayekutegemea.+
5 Kwa maana wewe, Ee Yehova, ni mwema+ na uko tayari kusamehe;+
Na fadhili zenye upendo ni nyingi kwa wale wote wanaokuitia.+
9 Mataifa yote ambayo umeyafanya, yatakuja yenyewe,+
Nayo yatainama mbele zako, Ee Yehova,+
Na kulipa utukufu jina lako.+
11 Unifundishe, Ee Yehova, juu ya njia yako.+
Nitatembea katika kweli yako.+
Unganisha moyo wangu ili kuliogopa jina lako.+
12 Ninakusifu, Ee Yehova Mungu wangu, kwa moyo wangu wote,+
Nami nitalitukuza jina lako mpaka wakati usio na kipimo,
13 Kwa maana fadhili zako zenye upendo ni kuu kunielekea mimi,+
Nawe umeikomboa nafsi yangu kutoka katika Kaburi,* mahali pake pa chini kabisa.+
14 Ee Mungu, wenye kimbelembele wamesimama juu yangu;+
Nalo kusanyiko la wenye kuonea wameitafuta nafsi yangu,+
Nao hawajakuweka mbele yao.+
15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na mwenye neema,+
Si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo na ukweli.+