Zaburi
Ya Daudi.
103 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,+
Naam, kila kitu kilicho ndani yangu, na kilibariki jina lake takatifu.+
2 Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu,
Wala usiyasahau matendo yake yote,+
3 Yeye anayesamehe makosa yako yote,+
Anayeponya magonjwa yako yote,+
4 Anayeuokoa uhai wako kutoka katika shimo,+
Anayekuvika taji la fadhili zenye upendo na rehema,+
5 Anayeushibisha muda wote wa maisha yako kwa mambo mema;+
Ujana wako unajifanya upya kama ule wa tai.+
8 Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema,+
Si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo.+
9 Yeye hataendelea kutafuta makosa wakati wote,+
Wala hataendelea kuweka kinyongo mpaka wakati usio na kipimo.+
10 Hakututendea kulingana na dhambi zetu;+
Wala kuleta juu yetu kile tunachostahili kulingana na makosa yetu.+
11 Kwa maana kama mbingu zilivyo juu kuliko dunia,+
Ndivyo fadhili zake zenye upendo zilivyo kuu kuwaelekea wale wanaomwogopa.+
12 Kama vile mashariki ilivyo mbali sana na magharibi,+
Ndivyo ameweka makosa yetu mbali sana na sisi.+
13 Kama vile baba anavyowaonyesha wanawe rehema,+
Ndivyo ambavyo Yehova amewaonyesha rehema wale wanaomwogopa.+
15 Naye mwanadamu anayeweza kufa, siku zake ni kama zile za majani mabichi;+
Yeye huchanuka kama ua la shambani.+
16 Kwa maana upepo unapita juu yake, nalo halipo tena;+
Napo mahali pake hapataendelea kulitambua tena.+
17 Lakini fadhili zenye upendo za Yehova ni za tangu wakati usio na kipimo mpaka wakati usio na kipimo+
Kuwaelekea wale wanaomwogopa,+
Na uadilifu wake kwa wana wa wana,+
18 Kuwaelekea wale wanaolishika agano lake+
Na kuwaelekea wale wanaoyakumbuka maagizo yake ili kuyafanya.+
19 Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni;+
Nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu.+