Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 15:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Naye akasema: “Ikiwa utaisikiliza kwa makini sauti ya Yehova Mungu wako na kufanya lililo sawa machoni pake na kutega sikio usikie amri zake na kushika masharti yake yote,+ sitaweka juu yako yoyote ya magonjwa yale niliyoweka juu ya Wamisri;+ kwa sababu mimi ni Yehova anayekuponya.”+

  • Kumbukumbu la Torati 7:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na Yehova atakuondolea kila ugonjwa; na yale magonjwa mabaya ya Misri unayoyajua,+ hatayaweka juu yako, naye atayaweka juu ya wote wanaokuchukia.

  • Zaburi 41:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Yehova mwenyewe atamtegemeza katika kitanda cha ugonjwa;+

      Kitanda chake chote hakika utakibadilisha wakati wa ugonjwa wake.+

  • Zaburi 147:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Anawaponya+ wenye mioyo iliyovunjika,+

      Naye anafunga sehemu zao zenye maumivu.+

  • Isaya 33:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Na hakuna mkaaji atakayesema: “Mimi ni mgonjwa.”+ Watu wanaokaa katika nchi hiyo watakuwa wamesamehewa kosa lao.+

  • Yeremia 17:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Uniponye, Ee Yehova, nami nitapona.+ Uniokoe, nami nitaokoka;+ kwa maana wewe ni sifa yangu.+

  • Yakobo 5:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na sala ya imani itamponya huyo asiyejisikia vizuri,+ na Yehova atamwinua.+ Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.+

  • Ufunuo 21:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Naye atafuta kila chozi+ kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena,+ wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.+ Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki