Kutoka
15 Wakati huo Musa na wana wa Israeli wakaanza kumwimbia Yehova wimbo huu na kusema yafuatayo:+
“Acheni nimwimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana.+
Farasi na mpandaji wake amewatupa baharini.+
2 Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,+ kwa maana yeye ndiye wokovu wangu.+
Huyu ndiye Mungu wangu, nami nitamsifu;+ Mungu wa baba yangu,+ nami nitamwinua juu.+
3 Yehova ni mtu wa vita+ anayetenda kiume. Yehova ndilo jina lake.+
4 Ametupa magari ya Farao na majeshi yake baharini.+
Na mashujaa wake wa vita walio bora wamezamishwa katika Bahari Nyekundu.+
5 Maji yenye kututumuka yaliwafunika;+ wakashuka ndani ya vilindi kama jiwe.+
6 Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, unajionyesha kuwa wenye nguvu katika uwezo,+
Mkono wako wa kuume, Ee Yehova, unaweza kumvunja-vunja adui.+
7 Na katika wingi wa ukuu wako wewe unaweza kuwatupa chini wale wanaosimama juu yako;+
Wewe unaituma hasira yako inayowaka, nayo inawateketeza kama majani makavu.+
8 Na kwa pumzi kutoka katika mianzi ya pua+ yako maji yalirundamana;
Yalisimama tuli kama bwawa la mafuriko;
Maji yenye kututumuka yaligandamana katika moyo wa bahari.
9 Adui alisema, ‘Nitafuatilia!+ Nitafikia!+
Nitagawa nyara!+ Nafsi yangu itajawa nazo!
Nitauchomoa upanga wangu! Mkono wangu utawafukuzia mbali!’+
11 Ni nani kati ya miungu aliye kama wewe, Ee Yehova?+
Ni nani aliye kama wewe, unayejionyesha kuwa mwenye nguvu katika utakatifu?+
Unayestahili kuogopwa+ kwa nyimbo za sifa,+ Unayefanya mambo ya ajabu.+
12 Uliunyoosha mkono wako wa kuume,+ nayo dunia ikawameza.+
13 Wewe katika fadhili zako zenye upendo umewaongoza watu ambao umewakomboa;+
Wewe katika nguvu zako hakika utawaongoza mpaka kwenye makao yako matakatifu.+
15 Wakati huo mashehe wa Edomu kwa kweli watasumbuka;
Nao wadhalimu wa Moabu, kutetemeka kutawashika.+
Wakaaji wote wa Kanaani kwa kweli watavunjika moyo.+
16 Woga na hofu zitaanguka juu yao.+
Kwa sababu ya ukuu wa mkono wako watatulia kama jiwe,
Mpaka watu wako+ wapite, Ee Yehova,
17 Utawaleta na kuwapanda katika mlima wa urithi wako,+
Mahali palipofanywa imara ambapo umetayarisha ili ukae,+ Ee Yehova,
Patakatifu,+ Ee Yehova, ambapo mikono yako imepafanya imara.
18 Yehova atatawala akiwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele.+
19 Farasi wa Farao+ pamoja na magari yake ya vita na askari wake wapanda-farasi walipoingia baharini,+
Ndipo Yehova alipoyarudisha maji ya bahari juu yao,+
Huku wana wa Israeli wakitembea juu ya nchi kavu katikati ya bahari.”+
20 Naye Miriamu nabii, dada ya Haruni,+ akachukua tari mkononi mwake;+ na wanawake wote wakaanza kutoka pamoja naye wakiwa na matari na kucheza dansi.+ 21 Naye Miriamu akawa akiwaitikia wanaume:+
Farasi na mpandaji wake amewatupa baharini.”+
22 Baadaye Musa akaondoa Israeli kutoka katika Bahari Nyekundu nao wakaenda katika nyika ya Shuri+ na kupiga mwendo kwa siku tatu nyikani, lakini hawakupata maji.+ 23 Mwishowe wakafika Mara,+ lakini hawakuweza kunywa maji ya Mara kwa sababu yalikuwa machungu. Ndiyo sababu alipaita jina Mara.+ 24 Nao watu wakaanza kunung’unika juu ya Musa,+ na kusema: “Tutakunywa nini?” 25 Kisha yeye akamlilia Yehova.+ Basi Yehova akamwelekeza kwenye mti fulani, naye akautupa ndani ya maji nayo maji yakawa matamu.+
Hapo Yeye akawawekea sharti na kesi ya kuhukumia na hapo akawatia katika jaribu.+ 26 Naye akasema: “Ikiwa utaisikiliza kwa makini sauti ya Yehova Mungu wako na kufanya lililo sawa machoni pake na kutega sikio usikie amri zake na kushika masharti yake yote,+ sitaweka juu yako yoyote ya magonjwa yale niliyoweka juu ya Wamisri;+ kwa sababu mimi ni Yehova anayekuponya.”+
27 Baada ya hapo wakafika Elimu, ambapo palikuwa na mabubujiko 12 ya maji na mitende 70.+ Basi wakapiga kambi hapo kando ya maji hayo.