4 Ndipo Yehova akamwambia Musa: “Tazama, nitawanyeshea mkate kutoka mbinguni;+ nao watu watatoka nje na kuokota kila mtu kiasi chake siku baada ya siku,+ ili nipate kuwajaribu iwapo watatembea katika sheria yangu au hapana.+
2 Nawe uikumbuke njia yote ambayo Yehova Mungu wako alikutembeza miaka hii 40 nyikani,+ ili kukunyenyekeza,+ kukujaribu+ apate kujua yaliyokuwa moyoni mwako,+ iwapo utashika amri zake au hapana.
7 ili sifa iliyojaribiwa ya imani+ yenu, iliyo na thamani kubwa zaidi kuliko dhahabu ambayo huharibika ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto,+ ipatikane kuwa sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo+ wa Yesu Kristo.