Kumbukumbu la Torati
8 “Kila amri ninayokuamuru leo muwe waangalifu kuishika,+ ili mpate kuendelea kuishi+ na kuongezeka, mwingie na kuimiliki nchi ambayo Yehova aliwaapia mababu zenu.+ 2 Nawe uikumbuke njia yote ambayo Yehova Mungu wako alikutembeza miaka hii 40 nyikani,+ ili kukunyenyekeza,+ kukujaribu+ apate kujua yaliyokuwa moyoni mwako,+ iwapo utashika amri zake au hapana. 3 Kwa hiyo alikunyenyekeza, akakuacha ukae na njaa,+ akakulisha mana,+ ambayo hukuwa umeijua wala baba zako hawakuwa wameijua; ili kukufanya ujue kwamba mwanadamu haishi kwa mkate tu bali mwanadamu huishi kwa kila neno la kinywa cha Yehova.+ 4 Nguo yako ya kujitanda haikuchakaa, wala mguu wako haukuvimba miaka hii 40.+ 5 Nawe unajua vema kwa moyo wako mwenyewe kwamba kama vile mtu anavyomrekebisha mwana wake, ndivyo Yehova Mungu wako alikuwa akikurekebisha.+
6 “Nawe ushike amri za Yehova Mungu wako kwa kutembea katika njia zake+ na kwa kumwogopa.+ 7 Kwa maana Yehova Mungu wako anakuleta katika nchi nzuri,+ nchi yenye mabonde ya mito yenye maji, mabubujiko na vilindi vya maji kutoka katika nchi tambarare ya bonde+ na katika eneo lenye milima, 8 nchi ya ngano na shayiri na mizabibu na tini na makomamanga,+ nchi ya mizeituni ya mafuta na asali,+ 9 nchi ambamo hutakula mkate kwa uhaba, ambamo hutakosa chochote, nchi ambayo mawe yake ni chuma na ambayo kutoka katika milima yake utachimba shaba.
10 “Utakapokuwa umekula na kushiba,+ wewe pia unapaswa kumbariki+ Yehova Mungu wako kwa ajili ya mema ya nchi ambayo amekupa.+ 11 Jiangalie usije ukamsahau+ Yehova Mungu wako kwa kutozishika amri zake na maamuzi yake ya hukumu na sheria zake ambazo ninakuamuru leo;+ 12 usije ukala na kushiba kwelikweli, ukajenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake,+ 13 na mifugo yako na kundi lako likaongezeka, na fedha na dhahabu zikakuongezekea, na vyote vilivyo vyako vikaongezeka; 14 nao moyo wako uinuke juu,+ na umsahau Yehova Mungu wako, aliyekutoa katika nchi ya Misri, kutoka katika nyumba ya watumwa;+ 15 aliyekutembeza katika ile nyika kubwa na yenye kuogopesha,+ iliyo na nyoka wenye sumu+ na nge na nchi kame ambayo haina maji; ambaye alikutolea maji katika jiwe gumu;+ 16 aliyekulisha mana+ nyikani, ambayo baba zako hawakuwa wameijua, apate kukunyenyekeza+ na kukujaribu ili akutendee mema siku zako za baadaye;+ 17 nawe useme moyoni mwako, ‘Nguvu zangu mwenyewe na uwezo kamili wa mkono wangu mwenyewe zimenifanyizia mali hii.’+ 18 Nawe umkumbuke Yehova Mungu wako, kwa sababu yeye ndiye anayekupa nguvu za kufanyiza mali;+ ili kutimiza agano lake ambalo aliwaapia mababu zako, kama ilivyo leo hii.+
19 “Na itatukia kwamba ikiwa utamsahau Yehova Mungu wako hata kidogo nawe ufuate miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia, nashuhudia juu yenu leo kwamba ninyi mtaangamia kabisa.+ 20 Kama yale mataifa ambayo Yehova anaangamiza kutoka mbele yenu, hivyo ndivyo mtakavyoangamia, kwa sababu ninyi hamtaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.+