Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 14:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 ‘Yehova, si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ anayesamehe kosa na ubaya,+ lakini ambaye kwa vyovyote hatakosa kuadhibu,+ anayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la baba juu ya wana, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne.’+

  • Kumbukumbu la Torati 5:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 lakini ninayeonyesha fadhili zenye upendo kwa kizazi cha elfu kwa wale wanaonipenda na wanaoshika amri zangu.+

  • Nehemia 9:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo wakakataa kusikiliza,+ wala hawakuyakumbuka+ matendo yako ya ajabu ambayo ulikuwa umewafanyia, bali wakafanya shingo zao kuwa ngumu+ na kujichagulia mkuu+ ili kurudi kwenye hali yao ya utumwa katika Misri. Lakini wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe,+ mwenye neema+ na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi+ wa fadhili zenye upendo, nawe hukuwaacha.+

  • Zaburi 86:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na mwenye neema,+

      Si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo na ukweli.+

  • Yeremia 32:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Wewe unayeonyesha fadhili zenye upendo kuelekea maelfu,+ na kulipa kosa la akina baba katika vifua vya wana wao baada yao,+ Mungu wa kweli, aliye Mkuu,+ Mwenye nguvu,+ Yehova wa majeshi+ ndilo jina lake,+

  • Yoeli 2:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu;+ rudini kwa Yehova Mungu wenu, kwa maana yeye ana neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ naye hakika atajuta kwa sababu ya msiba huo.+

  • Yona 4:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kwa hiyo akasali kwa Yehova na kusema: “Ah, sasa, Ee Yehova, je, hili halikuwa hangaiko langu, nilipokuwa katika nchi yangu mwenyewe? Ndiyo sababu nilikimbia na kwenda Tarshishi;+ kwa maana nilijua kwamba wewe ni Mungu mwenye neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ na mwenye kuujuta msiba.+

  • Nahumu 1:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Yehova si mwepesi wa hasira+ naye ni mkuu katika nguvu,+ wala hatasita kamwe kuadhibu.+

      Njia yake imo katika upepo wenye kuharibu na katika dhoruba, na wingu kubwa ndilo mavumbi ya miguu yake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki