Hesabu
14 Ndipo kusanyiko lote likapaaza sauti zao, nao watu wakazidi kupaaza sauti zao na kulia+ usiku kucha. 2 Na wana wote wa Israeli wakaanza kunung’unika juu ya Musa na Haruni,+ na kusanyiko lote likaanza kusema dhidi yao: “Laiti tungalikufa katika nchi ya Misri, au laiti tungalikufa katika nyika hii! 3 Na kwa nini Yehova anatuleta kwenye nchi hii ili tuanguke kwa upanga?+ Wake zetu na watoto wetu wadogo watakuwa nyara.+ Je, si afadhali kwetu turudi Misri?”+ 4 Hata wakaambiana: “Na tuchague kiongozi, nasi turudi Misri!”+
5 Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi+ mbele ya kutaniko lote la kusanyiko la wana wa Israeli. 6 Na Yoshua mwana wa Nuni+ na Kalebu mwana wa Yefune,+ ambao ni kati ya wale walioipeleleza nchi hiyo, wakayararua mavazi yao,+ 7 nao wakaliambia kusanyiko lote la wana wa Israeli hivi: “Nchi tuliyoipitia ili kuipeleleza ni nchi nzuri sana, sana.+ 8 Ikiwa Yehova amependezwa nasi,+ basi kwa hakika atatuingiza katika nchi hii na kutupa sisi, nchi inayotiririka maziwa na asali.+ 9 Ila tu msimwasi Yehova;+ nanyi msiwaogope watu wa nchi hiyo,+ kwa maana wao ni mkate kwetu. Ulinzi wao umegeuka kutoka juu yao,+ na Yehova yuko pamoja nasi.+ Msiwaogope.”+
10 Hata hivyo, kusanyiko lote likasema wapigwe kwa mawe.+ Na utukufu wa Yehova ukaonekana juu ya hema la mkutano machoni pa wana wote wa Israeli.+
11 Mwishowe Yehova akamwambia Musa: “Watu hawa wataendelea kunitendea bila heshima+ mpaka wakati gani,+ nao watakosa kuniamini mpaka wakati gani ijapokuwa ishara zote ambazo nilifanya katikati yao?+ 12 Acha niwapige kwa tauni na kuwafukuzia mbali, na acha nikufanye wewe kuwa taifa kubwa zaidi na lenye nguvu zaidi kuliko wao.”+
13 Lakini Musa akamwambia Yehova: “Ndipo hakika Wamisri watasikia kwamba kwa nguvu zako uliwaongoza watu hawa kutoka katikati yao.+ 14 Nao hakika watawaambia wakaaji wa nchi hii. Wamesikia kwamba wewe ni Yehova katikati ya watu hawa,+ ambaye umeonekana uso kwa uso.+ Wewe ni Yehova, nalo wingu lako linasimama juu yao, nawe unaenda mbele yao katika nguzo ya wingu wakati wa mchana na katika nguzo ya moto wakati wa usiku.+ 15 Ukiwaua watu hawa kama mtu mmoja,+ ndipo mataifa ambayo yamesikia juu ya sifa yako watasema hivi, 16 ‘Kwa sababu Yehova hakuweza kuwaleta watu hawa katika nchi ambayo aliwaapia, aliwaua nyikani.’+ 17 Na sasa, tafadhali, nguvu zako na ziwe kuu,+ Ee Yehova, kama ulivyonena, na kusema, 18 ‘Yehova, si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ anayesamehe kosa na ubaya,+ lakini ambaye kwa vyovyote hatakosa kuadhibu,+ anayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la baba juu ya wana, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne.’+ 19 Usamehe, tafadhali, kosa la watu hawa kulingana na ukuu wa fadhili zako zenye upendo, na kama vile ambavyo umewasamehe watu hawa tangu Misri na kuendelea mpaka sasa.”+
20 Ndipo Yehova akasema: “Ninasamehe kulingana na neno lako.+ 21 Na, kwa upande mwingine, kama ninavyoishi, dunia yote itajaa utukufu wa Yehova.+ 22 Lakini watu wote ambao wamekuwa wakiuona utukufu+ wangu na ishara+ zangu ambazo nimefanya katika Misri na nyikani na bado wakaendelea kunijaribu+ mara kumi hizi, nao hawakuisikiliza sauti yangu,+ 23 hawataiona kamwe nchi ambayo niliwaapia baba zao, naam, wale wote wanaonitendea bila heshima hawataiona.+ 24 Naye mtumishi wangu Kalebu,+ kwa sababu roho iliyo tofauti ilionekana kuwa pamoja naye, naye aliendelea kunifuata kikamilifu,+ nitamwingiza katika nchi ambamo ameenda, na wazao wake wataimiliki.+ 25 Huku Waamaleki na Wakanaani+ wakiwa wanakaa katika nchi tambarare ya chini, geukeni kesho na kuondoka ili mpige mwendo kuelekea nyikani kupitia njia ya Bahari Nyekundu.”+
26 Naye Yehova akasema na Musa na Haruni, na kumwambia: 27 “Kusanyiko hili lenye uovu litaendelea kuwa na manung’uniko haya ambayo linaendeleza juu yangu mpaka wakati gani?+ Nimesikia manung’uniko ya wana wa Israeli wanayonung’unika juu yangu.+ 28 Waambie, ‘ “Kama ninavyoishi,” asema Yehova, “ikiwa sitawafanyia ninyi vile ambavyo mmesema masikioni mwangu!+ 29 Katika nyika hii mizoga yenu itaanguka,+ naam, wote kati ya hesabu yenu ya walioandikishwa kuanzia miaka 20 na zaidi, ninyi ambao mmenung’unika juu yangu.+ 30 Nanyi hamtaingia katika nchi ambayo niliinua mkono wangu katika kiapo+ ya kwamba nitakaa pamoja nanyi, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.+
31 “‘“Nao watoto wenu wadogo mliosema watakuwa nyara,+ hao pia hakika nitawaingiza, nao kwa kweli wataijua nchi ambayo mmeikataa.+ 32 Lakini mizoga yenu wenyewe itaanguka katika nyika hii.+ 33 Na wana wenu watakuwa wachungaji nyikani+ kwa miaka 40, nao watajibu kwa sababu ya matendo yenu ya uasherati,+ mpaka mizoga yenu itakapofikia mwisho wake nyikani.+ 34 Kwa hesabu ya siku mlizoipeleleza nchi hiyo, siku 40,+ siku moja kwa mwaka mmoja, siku moja kwa mwaka mmoja,+ mtajibu kwa sababu ya makosa yenu miaka 40,+ kwa maana lazima mjue maana ya mimi kutenganishwa nanyi.+
35 “‘“Mimi Yehova nimesema hakika hilo ndilo nitakalolitendea kusanyiko hili lote lenye uovu,+ wale ambao wamekusanyika pamoja dhidi yangu: Katika nyika hii watafikia mwisho wao, na humo watakufa.+ 36 Na wale wanaume ambao Musa aliwatuma kuipeleleza nchi na ambao, waliporudi, walianza kulifanya kusanyiko lote linung’unike juu yangu, kwa kuleta habari mbaya juu ya nchi hiyo,+ 37 naam, wanaume walioleta habari mbaya juu ya nchi watakufa kwa tauni mbele za Yehova.+ 38 Lakini Yoshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune wataendelea kuishi, kati ya wale wanaume walioenda kuipeleleza nchi.”’”+
39 Musa alipowaambia wana wote wa Israeli maneno hayo, ndipo watu wakaanza kuomboleza sana.+ 40 Na zaidi ya hayo, wakaamka asubuhi na mapema na kujaribu kwenda juu ya mlima, wakisema: “Tazama, sisi tutapanda mpaka mahali ambapo Yehova alitaja. Kwa maana tumetenda dhambi.”+ 41 Lakini Musa akasema: “Kwa nini mnavunja agizo la Yehova?+ Lakini jambo hilo halitafanikiwa. 42 Msipande, kwa sababu Yehova hayuko katikati yenu, msije mkashindwa mbele ya adui zenu.+ 43 Kwa maana Waamaleki na Wakanaani wako huko mbele yenu;+ nanyi hakika mtaanguka kwa upanga, kwa sababu mligeuka na kuacha kumfuata Yehova, Yehova hataendelea kuwa pamoja nanyi.”+
44 Hata hivyo, wakafanya kimbelembele kupanda mpaka juu ya mlima,+ lakini sanduku la agano la Yehova na Musa hawakuondoka katikati ya kambi.+ 45 Ndipo Waamaleki+ na Wakanaani waliokuwa wakikaa katika mlima huo wakashuka na kuanza kuwapiga nao wakawatawanya mpaka Horma.+