Hesabu
13 Sasa Yehova akasema na Musa, na kumwambia: 2 “Tuma watu kwa ajili yako wapate kuipeleleza nchi ya Kanaani, ninayowapa wana wa Israeli.+ Mtamtuma mtu mmoja kwa ajili ya kila kabila la baba yake, kila mmoja wao mkuu+ kati yao.”
3 Basi Musa akawatuma kutoka katika nyika ya Parani+ kwa agizo la Yehova. Wanaume wote hao walikuwa vichwa vya wana wa Israeli. 4 Na haya ndiyo majina yao: Wa kabila la Rubeni, Shamua mwana wa Zakuri; 5 wa kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori; 6 wa kabila la Yuda, Kalebu+ mwana wa Yefune; 7 wa kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu; 8 wa kabila la Efraimu, Hoshea+ mwana wa Nuni; 9 wa kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu; 10 wa kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi; 11 wa kabila la Yosefu,+ kwa ajili ya kabila la Manase,+ Gadi mwana wa Susi; 12 wa kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali; 13 wa kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli; 14 wa kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofsi; 15 wa kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki. 16 Hayo ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma wakaipeleleze nchi. Na huyo Hoshea mwana wa Nuni, Musa akamwita Yehoshua.+
17 Musa alipokuwa akiwatuma kuipeleleza nchi ya Kanaani, aliwaambia: “Pandeni hapa na kuingia Negebu,+ nanyi mtapanda na kuingia katika eneo lenye milima.+ 18 Nanyi mtaona jinsi nchi ilivyo+ na watu wanaokaa humo, ikiwa wana nguvu au ni dhaifu, ikiwa ni wachache au ni wengi; 19 na jinsi nchi wanayokaa ndani yake ilivyo, iwapo ni nzuri au ni mbaya, na jinsi majiji wanayokaa ndani yake yalivyo, iwapo ni katika kambi au ni katika ngome; 20 Na jinsi nchi ilivyo, iwapo ni nono au imekonda,+ iwapo kuna miti ndani yake au hakuna. Nanyi mjionyeshe kuwa hodari+ na kuchukua baadhi ya matunda ya nchi hiyo.” Sasa siku hizo zilikuwa siku za matunda yaliyoiva ya kwanza ya zabibu.+
21 Basi wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka katika nyika ya Zini+ mpaka Rehobu+ mpaka mahali pa kuingilia pa Hamathi.+ 22 Walipopanda kuingia Negebu,+ ndipo wakafika Hebroni.+ Sasa Ahimani, Sheshai na Talmai,+ wale waliozaliwa kwa Anaki+ walikuwa huko. Hebroni+ lilikuwa limejengwa miaka saba kabla ya Soani+ la Misri. 23 Walipofika kwenye bonde la mto la Eshkoli,+ wakakata chipukizi lenye kishada kimoja cha zabibu.+ Na wawili kati ya wanaume hao wakalichukua kwa ufito, na pia baadhi ya makomamanga+ na baadhi ya tini. 24 Wakapaita mahali hapo bonde la mto la Eshkoli,+ kwa sababu ya kile kishada ambacho wana wa Israeli walikata kutoka huko.
25 Mwishowe, mwishoni mwa siku 40+ wakarudi kutoka kuipeleleza nchi. 26 Basi wakatembea na kuja kwa Musa na Haruni na kusanyiko lote la wana wa Israeli katika nyika ya Parani, huko Kadeshi.+ Nao wakaleta neno kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya nchi. 27 Nao wakampa habari na kusema: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo kwa kweli inatiririka maziwa na asali,+ na haya ni matunda yake.+ 28 Hata hivyo, mambo ya hakika ni kwamba watu wanaokaa katika nchi hiyo ni wenye nguvu, na majiji yenye ngome ni makubwa sana;+ na, pia, wazao wa Anaki tuliwaona huko.+ 29 Waamaleki+ wanakaa katika nchi ya Negebu,+ na Wahiti na Wayebusi+ na Waamori+ wanakaa katika eneo lenye milima, na Wakanaani+ wanakaa kando ya bahari na kando ya ukingo wa Yordani.”
30 Ndipo Kalebu+ akajaribu kuwatuliza watu mbele ya Musa naye akasema: “Na tupande moja kwa moja, nasi tutaimiliki, kwa sababu kwa hakika tunaweza kuishinda.”+ 31 Lakini wale watu waliopanda pamoja naye wakasema: “Hatuwezi kupanda kupigana na watu hao, kwa sababu ni wenye nguvu kuliko sisi.”+ 32 Nao wakazidi kuwaletea wana wa Israeli habari mbaya+ juu ya nchi waliyokuwa wameipeleleza, na kusema: “Ile nchi, tuliyoipitia ili kuipeleleza, ni nchi ambayo inakula wakaaji wake; na watu wote tuliowaona katikati yake ni watu wenye ukubwa usio wa kawaida.+ 33 Na humo tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki,+ waliotoka kwa Wanefili; hivi kwamba sisi tukawa machoni petu wenyewe kama panzi, na machoni pao sisi tukawa vivyo hivyo.”+