Zaburi
Ya Daudi.
3 Na uchomoe mkuki na shoka lenye makali kuwili ili kukutana na wale wanaonifuatilia.+
Uiambie nafsi yangu: “Mimi ni wokovu wako.”+
4 Wale wanaoiwinda nafsi yangu na waone aibu na kufedheheka.+
Wale wanaonipangia hila nipatwe na msiba na warudishwe nyuma na kufedheheka.+
7 Kwa maana wamenifichia bila sababu shimo lao lenye wavu;+
Wamelichimba bila sababu kwa ajili ya nafsi yangu.+
8 Uharibifu na umjie bila yeye kujua,+
Na wavu wake mwenyewe aliouficha na umkamate;+
Na aanguke ndani yake apatwe na uharibifu.+
10 Mifupa yangu yote na iseme:+
“Ee Yehova, ni nani aliye kama wewe,+
Anayemkomboa mwenye kuteseka kutoka kwa mwenye nguvu kuliko yeye,+
Na kumkomboa mwenye kuteseka na maskini kutoka kwa mwenye kumnyang’anya?”+
13 Lakini mimi, walipokuwa wagonjwa, mavazi yangu yalikuwa ni magunia,+
Nikaitesa nafsi yangu kwa kufunga,+
Nayo sala yangu mwenyewe ikawa ikirudi kifuani pangu.+
14 Kana kwamba ni kwa ajili ya mwenzangu, kana kwamba ni kwa ajili ya ndugu yangu,+
Nilitembea huku na huku kama mtu anayemwombolezea mama yake.+
Nikainama nikiwa na huzuni.
15 Lakini walishangilia na kukusanyika pamoja kuhusu kuchechemea kwangu;+
Walikusanyika pamoja dhidi yangu,+
Wakinipiga na kuniangusha wakati sikujua;+
Walinirarua vipande-vipande wala hawakukaa kimya.+
16 Kati ya wenye dhihaka, walioasi imani, kwa ajili ya keki,+
Kulikuwako kusaga meno yao dhidi yangu.+
17 Ee Yehova, utaendelea kuona hayo mpaka wakati gani?+
Uirudishe nafsi yangu kutoka katika maangamizi yao,+
Naam, yangu iliyo ya pekee+ kutoka kwa wana-simba wenye manyoya shingoni.
19 Wale ambao ni adui zangu bila sababu yoyote wasishangilie juu yangu;+
Nao wale wanaonichukia bila sababu, wasikonyeze jicho.+
20 Kwa maana hawasemi mambo ya amani;+
Bali juu ya wanyamavu wa dunia
Wanaendelea kupanga mambo ya udanganyifu.+
23 Uamke na ukae macho kwa ajili ya hukumu yangu,+
Kwa ajili ya kesi yangu,+ Ee Mungu wangu, naam, Yehova.
26 Na waone aibu na kufedheheka wote pamoja+
Wanaoshangilia msiba wangu.+
Na wavikwe aibu+ na fedheha wale wanaojivuna sana dhidi yangu.+