4 Kwa kweli mlikuwa mkifunga kwa kusudi la kugombana na kupambana,+ na kwa kusudi la kupiga kwa ngumi ya uovu.+ Je, hamkuendelea kufunga kama katika siku ile ya kufanya sauti yenu isikike kileleni?
16 “Wakati mnapofunga,+ msiwe na nyuso zenye huzuni kama wanafiki, kwa maana wao hukunja nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga.+ Kwa kweli ninawaambia ninyi, Wanapata thawabu yao kwa ukamili.
23 Kwa kweli, mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima katika namna ya ibada ya kujitwika mwenyewe na unyenyekevu wa kujifanya, kuutendea mwili kwa ukali;+ lakini hayana thamani yoyote katika kuzuia kuutosheleza mwili.+