-
Marko 16:8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
8 Kwa hiyo walipotoka wakakimbia kutoka kwenye kaburi, kwa maana walikuwa wakitetemeka nao walikuwa na hisia nyingi. Nao hawakumwambia mtu jambo lolote, kwa maana walikuwa wanaogopa.+
UMALIZIO MFUPI
Hati na tafsiri fulani za mwisho-mwisho zina umalizio mfupi baada ya Marko 16:8, kama ifuatavyo:
Lakini mambo yote yaliyokuwa yameamriwa wakayasimulia kwa ufupi kwa wale waliomzunguka Petro. Tena, baada ya mambo hayo, Yesu mwenyewe akapeleka kupitia wao tangazo takatifu na lisiloweza kuharibika la wokovu wa milele kutoka mashariki mpaka magharibi.
-