9 Hata hivyo, ninyi hampatani na mwili, bali mnapatana na roho,+ ikiwa kweli roho ya Mungu inakaa ndani yenu.+ Lakini ikiwa mtu yeyote hana roho+ ya Kristo, mtu huyo si wake.
23 Si hilo tu, bali sisi wenyewe pia tulio na matunda ya kwanza,+ yaani, ile roho, ndiyo, sisi wenyewe tunaugua+ ndani yetu wenyewe, huku tukingojea kwa bidii kufanywa kuwa wana,+ kuachiliwa huru kutoka katika miili yetu kwa njia ya fidia.
13 Kwa kweli kwa roho moja sote tulibatizwa+ katika mwili mmoja, kama ni Wayahudi au ni Wagiriki, kama ni watumwa au ni walio huru, nasi sote tulinyweshwa+ roho moja.