Ya wana wa Kora. Muziki, wimbo.
87 Msingi wake uko katika milima mitakatifu.+
2 Yehova anapenda zaidi malango ya Sayuni+
Kuliko maskani zote za Yakobo.+
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, Ee jiji la Mungu wa kweli.+ Sela.
4 Nitataja Rahabu na Babiloni+ kuwa kati ya wale wanaonijua mimi;
Tazama, Ufilisti+ na Tiro, pamoja na Kushi:+
“Huyu alizaliwa humo.”+
5 Na juu ya Sayuni itasemwa:
“Kila mmoja alizaliwa humo.”+
Na Aliye Juu Zaidi+ atamfanya imara.+
6 Yehova mwenyewe atatangaza, anapoandikisha vikundi vya watu:+
“Huyu alizaliwa humo.”+ Sela.
7 Pia kutakuwako waimbaji na vilevile wachezaji wa dansi za mzunguko:+
“Mabubujiko yangu yote yamo ndani yako.”+