-
Mwanzo 37:7-9Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
7 Tulikuwa tukifunga matita ya masuke katikati ya shamba kisha tita langu likainuka na kusimama wima, nayo matita yenu yakalizunguka tita langu na kuliinamia.”+ 8 Ndugu zake wakamuuliza: “Je, kweli utajiweka kuwa mfalme wetu na kututawala?”+ Basi wakapata sababu nyingine ya kumchukia, kwa sababu ya ndoto zake na mambo aliyosema.
9 Baada ya hayo akaota tena ndoto nyingine, naye akawasimulia ndugu zake ndoto hiyo: “Nimeota ndoto nyingine. Wakati huu jua na mwezi na nyota 11 zilikuwa zikiniinamia.”+
-