-
Mwanzo 37:34, 35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
34 Ndipo Yakobo akayararua mavazi yake na kuvaa nguo za magunia kiunoni na kumwombolezea mwanawe kwa siku nyingi. 35 Na wanawe wote na mabinti zake wote wakajaribu sana kumfariji, lakini alikataa kabisa kufarijiwa, akisema: “Nitashuka Kaburini*+ nikimwombolezea mwanangu!” Na baba yake akaendelea kumlilia.
-
-
Mwanzo 46:30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Sasa niko tayari kufa; nimeona uso wako na kujua kwamba ungali hai.”
-