Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 3:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Nami nitaweka uadui*+ kati yako+ na mwanamke+ na kati ya uzao wako*+ na uzao wake.*+ Yeye atakuponda* kichwa,+ nawe utamuuma* kisigino.”+

  • Mwanzo 21:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kisha Mungu akamwambia Abrahamu: “Usikasirishwe na jambo ambalo Sara anakuambia kuhusu mvulana huyo na kuhusu kijakazi wako. Msikilize,* kwa maana ule utakaoitwa uzao wako utapitia* kwa Isaka.+

  • Mwanzo 28:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Na tazama! Yehova alikuwa amesimama juu yake, naye akasema:

      “Mimi ni Yehova Mungu wa Abrahamu baba yako na Mungu wa Isaka.+ Nchi unayoilalia, nitakupa wewe na uzao wako.*+ 14 Na hakika uzao wako utakuwa kama chembe za mavumbi ya ardhi,+ nawe utaenea mpaka upande wa magharibi na upande wa mashariki na upande wa kaskazini na upande wa kusini, na kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote duniani hakika zitabarikiwa.*+

  • Waroma 9:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Wala si wote walio watoto kwa sababu wao ni uzao wa* Abrahamu;+ badala yake, “Ule utakaoitwa uzao wako* utapitia kwa Isaka.”+

  • Wagalatia 3:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Sasa ahadi zilitolewa kwa Abrahamu na kwa uzao wake.*+ Haisemi, “na kwa wazao wako,”* kana kwamba ni wengi. Badala yake, inasema, “na kwa uzao wako,”* kana kwamba ni kwa mmoja, ambaye ni Kristo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki