Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 13:14, 15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Yehova akamwambia hivi Abramu baada ya Loti kujitenga naye: “Tafadhali, inua macho yako, na kutoka mahali ulipo tazama kaskazini na kusini, mashariki na magharibi, 15 kwa sababu nchi yote unayoona, nitakupa wewe na uzao wako* iwe miliki yenu ya kudumu.+

  • Mwanzo 15:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Baada ya hayo neno la Yehova likamjia Abramu katika maono, likisema: “Usiogope,+ Abramu. Mimi ni ngao yako.+ Thawabu yako itakuwa kubwa sana.”+

  • Mwanzo 15:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Pia akasema hivi: “Mimi ni Yehova, niliyekutoa katika jiji la Uru la Wakaldayo ili nikupe nchi hii iwe miliki yako.”+

  • Mwanzo 17:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Abramu alipokuwa na umri wa miaka 99, Yehova alimtokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu Mweza-Yote. Tembea mbele zangu na ujithibitishe mwenyewe kuwa bila kosa.*

  • Mwanzo 17:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Nami nitakupa wewe na uzao wako* baada yako nchi ambamo uliishi ukiwa mgeni+—nchi yote ya Kanaani—iwe miliki ya kudumu, nami nitakuwa Mungu wao.”+

  • Kumbukumbu la Torati 34:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Kisha Yehova akamwambia hivi: “Hii ndiyo nchi ambayo nilimwapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo, niliposema, ‘Nitaupa uzao wako* nchi hii.’+ Nimekuruhusu uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hutavuka kuingia humo.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki