Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 17:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Hili ndilo agano langu nililofanya pamoja nawe, ambalo wewe na uzao wako* baada yako mtalishika: Kila mwanamume miongoni mwenu ni lazima atahiriwe.+

  • Mwanzo 17:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Kisha Abrahamu akamchukua Ishmaeli mwana wake na wanaume wote waliozaliwa nyumbani mwake na kila mwanamume aliyekuwa amemnunua kwa pesa, kila mwanamume katika nyumba ya Abrahamu, naye akawatahiri nyama ya magovi yao siku hiyohiyo, kama Mungu alivyokuwa amemwambia.+

  • Mwanzo 22:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kwa hiyo Abrahamu akaamka asubuhi na mapema, akaweka matandiko juu ya punda wake na kuchukua wawili kati ya watumishi wake pamoja na Isaka mwanawe. Akapasua kuni kwa ajili ya dhabihu ya kuteketezwa, kisha akafunga safari kwenda mahali ambapo Mungu wa kweli alimwonyesha.

  • Mwanzo 22:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Kisha akasema: “Usimdhuru mvulana huyo, wala usimtendee lolote, kwa maana sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu kwa sababu hukuninyima+ mwana wako, mwana wako wa pekee.”

  • Waebrania 11:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kwa imani, Abrahamu+ alipoitwa alitii kwa kutoka na kwenda mahali ambapo angepokea kuwa urithi; aliondoka, ingawa hakujua mahali alipokuwa akienda.+

  • Yakobo 2:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Je, Abrahamu baba yetu hakutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo baada ya kumtoa Isaka mwana wake juu ya madhabahu?+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki