-
Kutoka 34:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Muwe waangalifu msifanye agano na wakaaji wa nchi, kwa maana wanapofanya ukahaba na miungu yao na kuitolea dhabihu,+ mmoja wao atawaalika nanyi mtakula dhabihu yake.+ 16 Kisha kwa hakika mtawachukua baadhi ya mabinti wao ili waolewe na wana wenu,+ na mabinti wao watafanya ukahaba na miungu yao na kusababisha wana wenu wafanye ukahaba na miungu yao.+
-
-
1 Wafalme 11:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Lakini mbali na binti ya Farao,+ Mfalme Sulemani aliwapenda wanawake wengi wa kigeni:+ wanawake Wamoabu,+ Waamoni,+ Waedomu, Wasidoni,+ na Wahiti.+ 2 Walitoka katika mataifa ambayo Yehova alikuwa amewaambia hivi Waisraeli kuyahusu: “Hampaswi kuingia miongoni mwao,* nao hawapaswi kuingia miongoni mwenu; kwa maana kwa hakika wataigeuza mioyo yenu ifuate miungu yao.”+ Lakini Sulemani alishikamana nao na kuwapenda. 3 Naye alikuwa na wake 700 waliokuwa mabinti wa wafalme na masuria 300, na hatua kwa hatua wake zake wakaugeuza moyo wake.*
-