Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 35:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Siku moja, Israeli alipokuwa akiishi katika nchi hiyo, Rubeni alienda na kulala na Bilha suria wa baba yake, naye Israeli akasikia habari hizo.+

      Basi Yakobo alikuwa na wana 12.

  • Mwanzo 37:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kisha akawaambia: “Msimwage damu.+ Mtupeni ndani ya shimo hili la maji lililo nyikani, lakini msimdhuru.”*+ Rubeni alikusudia kumwokoa kutoka mikononi mwao ili amrudishe kwa baba yake.

  • Mwanzo 49:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Rubeni,+ wewe ndiye mzaliwa wangu wa kwanza,+ nguvu zangu na mwanzo wa nguvu zangu za uzazi, ubora wa heshima na ubora wa nguvu. 4 Kwa vurugu kama maji yenye msukosuko, hutafanikiwa, kwa sababu ulikipanda kitanda cha baba yako.+ Wakati huo ulikichafua* kitanda changu. Kwa kweli alikipanda kitanda changu!

  • Kutoka 6:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Hawa ndio viongozi wa nyumba ya baba zao: Wana wa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ Hizo ndizo koo za Rubeni.

  • 1 Mambo ya Nyakati 5:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Hawa ndio wana wa Rubeni,+ mzaliwa wa kwanza wa Israeli. Yeye ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza, lakini kwa sababu alikichafua* kitanda cha baba yake,+ haki yake ya mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yosefu+ mwana wa Israeli, kwa hiyo hakuandikishwa katika orodha ya ukoo kwamba ana haki ya mzaliwa wa kwanza.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki